Sunday, October 9, 2011

Poulsen ataja First XI

Taifa Stars
Kocha Jan Poulsen ametaja kikosi cha wachezaji 11 ambao wataanza kwenye mechi ya leo dhidi ya Morocco. Mechi hiyo inaanza saa 1.30 usiku kwa saa za hapa ambapo nyumbani Tanzania ni saa 4.30 usiku na itachezwa Grand Stadium hapa Marrakech. Poulsen atatumia mfumo wa 4-4-1-1 huku akimweka Mbwana Samata kuwa mshambuliaji wa mwisho na nyuma yake akicheza Abdi Kassim.
Katika kikosi cha kwanza amewaanzisha wachezaji wote wa kulipwa wanaocheza nje ya Tanzania ambao anao hapa. Amewataka wachezaji kuwa focussed na mchezo, kujituma na kila mmoja kutekeleza wajibu wake uwanjani ili ushindi uweze kupatikana. Baada ya kutoa game plan yake, Poulsen aliwaonesha wachezaji CD ya mechi ya kwanza nyumbani dhidi ya Morocco ambapo tulifungwa bao 1-0.
Kupitia CD hiyo aliwaeleza wachezaji upungufu uliojitokeza na pia wachezaji hatari wa Morocco wanaotakiwa kuangaliwa kutokana na uzuri wao wanapokuwa uwanjani. Amewakumbusha mabeki kuwa mshambuliaji Chamakh Marouane (Arsenal, Uingereza) kuwa ni mzuri kwa mipira ya vichwa, hivyo kutomuacha kuruka peke yake katika mipira hiyo.
Stars: Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Idrisa Rajab, Juma Nyoso, Aggrey Morris, Shabani Nditi, Mohamed Rajab, Henry Joseph (Captain), Mbwana Samata, Abdi Kassim na Dan Mrwanda.

Subs: Shabani Dihile, Nassoro Cholo, John Bocco, Ramadhan Chombo, Mrisho Ngasa, Nadir Haroub, Jabir Aziz

Iniesta nje Mwezi Mmoja


 
 
Klabu ya Barcelona imetangaza kwenye mtandao wake kwamba, Andres Iniesta atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa mwezi mmoja.

Kiungo huyo aliumia dakika 5 kabla ya mapumziko, kwenye mechi ambayo timu yake ilitoka sare ya 2-2 na AC Milan, katika michuano ya Kombe la mabingwa Barani Ulaya siku ya Jumanne.

Iniesta atakosa mechi dhidi ya Osasuna, Valencia, Atletico Madrid, BATE Borisov na Sporting Gijon.

Mchezaji huyo anategemea kurudi tena uwanjani kwenye mechi ya michuano ya Euro 2012, ambapo timu ya Hispania itakapocheza na Czech Republic na Scotland, mnamo tarehe 7 na 11 Oktoba.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27, ameweza kucheza jumla ya mechi 6 kwa klabu msimu huu, huku akikamilisha wastani wa dakika 469 uwanjani.

Bradley aajiriwa Misri

 
 
Inaarifiwa kwamba, Kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Marekani Bob Bradley, ameajiliwa kuwa kocha wa timu ya taifa ya Misri.

Msemaji wa EFA Azmy Megahed amesema, Bradley anategemea kuwasili Cairo wikiendi hii kukamilisha mpango huo.

"Kila kitu kipo sawa. Bradley atawasili hapa siku ya Jumapili kukamilisha mkataba," Megahed alisema.

Bradley atakuwa amechukua nafasi ya kocha wa kipindi kirefu wa timu hiyo Hassan Shehata, ambaye kibarua chake kilisitishwa mnamo mwezi June, kufuatia kufanya vibaya kwa timu hiyo kwenye kampeni zake za kushiki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2012.

Timu hiyo mpaka sasa imetolewa kwenye mbio hizo.

Bradley aliiwezesha Marekani kufika kwenye mzunguko wa 16 wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010, iliyofanyika nchini Afrika ya Kusini.

Na alipigwa chini mnamo mwezi July baada ya Marekani kufungwa 4-2 na Mexico kwenye fainali ya Gold Cup, huku nafasi yake ikichukuliwa na kocha wa zamani wa Ujerumani Jurgen Klinsmann.

Bradley atakuwa na mtihani mzito kuhakikisha nchi ya Misri inapata nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia, kwa mara ya mwisho Taifa hilo kushiriki Kombe hilo ilikuwa ni mwaka 1990.
.
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Polisi Dodoma iliyochezwa Septemba 14 mwaka huu Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam imeingiza sh. 16,839,000.

Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo walikuwa 2,257 ambapo kiingilio kilikuwa sh, 7,000 kwa mzunguko na sh. 20,000 kwa VIP. Waliokata tiketi za sh. 20,000 walikuwa 80.

Baada ya kuondoa gharama za mchezo na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 2,568,661.02 kila timu ilipata sh. 3,546,671.90. Mgawo mwingine ulikwenda kwa uwanja (sh. 1,162,893.90), TFF (sh. 1,162,893.90), Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu- FDF (sh. 581,446.95), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam- DRFA (sh. 465,157.56) na Baraza la Michezo la Taifa- BMT (sh. 116,289.39).
Wayne Rooney
 
Meneja wa klabu ya Manchester United Sir Alex Ferguson, amemfananisha mshambuliaji wa timu yake Wayne Rooney na mchezaji mkongwe wa Brazil Pele.

Fergie ameyasema hayo, kuelelekea kwenye mechi ya Kombe la Klabu Bingwa ya Ulaya dhidi ya Benfica, mechi inayotarajiwa kuchezwa usiku huu, huku mchezaji huyo akionekana kuwa kwenye kiwango kizuri kiuchezaji.

Upatikanaji wa Tiketi mechi za Simba na Yanga Uwanja wa Chamazi

Tiketi kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu ya Vodacom zinazohusisha timu za Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam hazitauzwa uwanjani. Lengo ni kuwaondolea usumbufu mashabiki ambao wanakwenda kwenye mechi hizo na kukuta tiketi zimekwisha, hivyo kuweza kuwa chanzo cha vurugu.

Ili kujiridhisha Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lilifanya uhakiki na kubaini Uwanja wa Azam una uwezo wa kuchukua watazamaji 5,000 tu na si 7,000 kama ilivyoelezwa awali. Hata hivyo lengo la mmiliki wa uwanja huo ni kuongeza viti hadi kufikia 7,500.

Kwa mantiki hiyo tiketi zitakazouzwa kwa mechi za Yanga na Simba kwenye uwanja huo ni 5,000 tu. Vituo vya kuuzia tiketi hizo siku moja kabla ya mchezo na siku yenyewe ya mchezo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Kituo cha Mafuta cha OilCom kilichoko Ubungo na Mbagala Rangitatu.

Viingilio kwa mechi za timu hizo zitakazochezwa Uwanja wa Azam ni sh. 20,000 kwa jukwaa kuu lenye uwezo wa kuchukua watazamaji 400 wakati majukwaa ya kawaida itakuwa sh. 7,000. Ili kuhakikisha idadi ya mashabiki haizidi uwezo wa uwanja hakutakuwa na tiketi za bure (complimentary).

Hivyo kutokana na kuwepo vituo vya kuuzia tiketi katika maeneo yaliyotajwa, mashabiki ambao watakosa tiketi hawana sababu ya kwenda uwanjani. Simba na Yanga zitaanza kuutumia uwanja huo kesho (Septemba 14 mwaka huu) kwa Simba kuwa mwenyeji wa Polisi Dodoma wakati siku inayofuata Yanga itakuwa mgeni wa African Lyon.

Sendeu kwa Pilato Tibaigana

Luis Sendeu
 
Sekretarieti ya TFF itawasilisha mashtaka dhidi ya Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi inayoongozwa na Kamishna wa Polisi mstaafu Alfred Tibaigana kutokana na matamshi yake dhidi ya mwamuzi Alex Mahagi.

Mara baada ya mechi kati ya Yanga na Ruvu Shooting iliyochezwa Septemba 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1, Sendeu aliita mkutano na waandishi wa habari na kumshutumu Mahagi kuwa alisababisha timu yake ikose ushindi kwa kuwabeba wapinzani wao.

Aliongeza kuwa anamfahamu Mahagi kuwa ni mwanachama wa Simba, kadi nyekundu aliyompa kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima si halali na alifanya hivyo kwa lengo la kuisadia Simba ili iendelee kukaa kileleni mwa ligi.

Kauli ya Sendeu ililenga kumjengea chuki Mahagi mbele ya mashabiki wa Yanga kama ilivyo kwa viongozi na watendaji wa TFF. Ni wazi Sendeu akiwa ofisa wa Yanga anajua taratibu za kufanya pale klabu yake isiporidhishwa na uamuzi wa mwamuzi au suala lingine lolote.

Matamshi ya Sendeu yanalenga kuchochea chuki na vurugu katika mpira wa miguu ambapo ni kinyume na Ibara ya 53(1) na (2) ya Kanuni za Nidhamu za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Monday, September 5, 2011

Santos: Hakuna makubaliano ya kuuzwa Neymer

Neymar

Klabu ya Santos  ya nchini Brazil imesema haijafikia makubaliano na timu yoyote juu ya uwezekano wa kumuuza mshambuliaji wake Neymar.

Klabu hiyo imetoa tamko hilo Jumapili kwenye taarifa ndefu waliyoitoa kwenye Mtandao wake, taarifa hiyo imesisitiza kwamba, hakuna dili yoyote ambayo wamefikia na Barcelona juu ya kumuhamisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19, kwenda Camp Nou ifikapo mwaka 2013.

"Kutokana na sababu binafsi zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari hivi karibuni kuhusiana na Neymar, Santos Futebol Clube inapenda kutoa tamko rasmi kwamba, maelezo yanayotolewa na vyombo hivyo juu ya mustakabali wa Neymer sio za kweli” taarifa hiyo ilisema.

"Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu mara zote imekuwa na nia njema ya kuendelea kubaki na Neymer kwenye timu.”

Taarifa hiyo imekuja baada ya gazeti la Estadao siku ya Jumamosi kuandika kwamba, Santos na Barcelona wamefikia makubaliano ya awali kwa Neymar kujiunga na mabingwa Hispania na Ulaya baada ya miaka miwili toka sasa.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Bazil amekuwa akihusishwa na kuhamia Barcelona na pia kwa mahasimu wao Real Madrid katika kipindi cha majira ya joto, huku baadhi ya timu nyingine za Bara la Ulaya zikihusishwa juu ya mpango huo, ila mchezaji juyo amekuwa akisisitiza kwamba kwa muda huu angependa kuendelea kucheza nchini mwake.

Del Piero: Bado sijaamua mwisho wangu

Alessandro Del Piero

Mchezaji mkongwe wa Juventus Alessandro Del Piero, amesema bado hajaamua kama ataendelea kucheza mpira baada ya msimu huu wa 2011-12.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36, bado yupo kwenye mkataba unaomuweka mpaka mwezi June mwakani pale Turin, ila inaelezwa kwamba mwisho wa mkataba huo haimaanishi kwamba na yeye atastaafu.

"Kufikiria juu ya mwisho wangu kwenye soka , si kitu ambacho kinanichukulia muda kuamua. Bado sijaamua kama huu utakuwa ni mwisho wangu kucheza na Juventus," Del Piero alieleza La Gazzetta dello Sport.

"Kufikiria juu ya kwamba huu ni mwaka wangu wa mwisho inanifanya nijitoe kwa zaidi ya asilimia 200. Nahitaji kumaliza kipindi changu kwenye mafanikio ya juu.  Nikijaribu kuangalia nyuma miaka 20 iliyopita, nitaangalia nikiwa nimeridhika sana."

Del Piero alianza kucheza kwenye kiwango cha juu akiwa Padova, ila akajiunga na Juventus mnamo mwaka 1993. Mchezaji huyo mpaka sasa ameweza kucheza jumla ya mechi 600 kwa timu hiyo ya Serie A.

Capello: Barcelona Watafungika

Fabio Capello

Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza Fabio Capello amesema kwamba, anaamini haitachukua muda kwa timu ntingine kupata jibu juu ya aina ya mpira ambao timu ya Barcelona inaucheza.

Timu hiyo ya Catalans inaaminika na watu wengi kwamba ni timu kali ambayo haijawahi  tokea duniani, ila Capello anaamini kwamba utawala wao hautakuwa wa milele.

"Naweza kumuona mtu anayeweza kuizuia Barcelona kwa siku za mbele? Nafikiri ndio. Itawezekana, sababu tuna bahati kwamba tunaweza kuwasoma wapinzani," Capello alinikuliwa kwenye mtandao wa FIFA.
"Utapata ufumbuzi wa namna ya kuizuia Barcelona, kwa kuelewa uwezo wao. Utajifunza mengi, ukiangalia mchezo wao kwenye mikanda. Naamini baadhi ya timu zitapata dawa ya kuifunga."

Pia anaamini kwamba taratibu kama ilivyo asili ya mchezo kiwango chao kinaweza kushuka.

Akaendelea kusema "Unapokuwa unashinda mara nyingi, wakati mwengine  unakuwa unakosa kitu kinachokufanya uwe makini kwa kila mchezo kuweza kushinda, wachezaji wengine pia wanazeeka kimchezo."

Barcelona wameshinda Kombe la Mabingwa Ulaya msimu uliopita, na wameanza msimu mpya wa 2011-12, wakiwafunga wapinzani wao Real Madrid kwenye Supercup ya nchini kwao Hispania, halafu wakaja kuwafunga Porto kwenye Supercup ya Ulaya.

Mchezaji Bora wa Wiki Goal.com

Cesc Fabregas

Cesc Fabregas Mchezaji Bora wa Wiki Goal.com
Klabu: Barcelona

Nchi:Hispania

Miaka: 24
Nafasi: Kiungo

Mafanikio: Amesaidia ushindi kwa Barcelona na timu ya Taifa ya Hispania

Terry: Don't write off Lampard


England captain John Terry has voiced his full support for dropped midfielder Frank Lampard.

An injury-free Lampard was left out of a competitive England starting XI for the first time since 2007 with a midfield trio of Scott Parker, Gareth Barry and Ashley Young preferred for the 3-0 Euro 2012 qualifier win over Bulgaria last Friday.

There have been suggestions that Lampard's exclusion could be the beginning of the end of the 33-year-old's international career, but his Chelsea team-mate Terry has issued a warning to the doubters.

Speaking ahead of Tuesday's meeting with Wales at Wembley, Terry said: "Write Frank Lampard off at your peril. I have known him an awful long time and he was disappointed about not starting but trained incredibly hard the day after and he remains one of the best players I have ever played with.

"Because of his age people tend to write him off but he is still in excellent form. His record for England has been incredible.''

Twiga Stars yalala dhidi ya Ghana

 
 
Timu ya wanawake ya Taifa ya Tanzania (Twiga Stars) imepoteza mechi yake ya kwanza ya michezo ya All Africa Games (AAG) baada ya leo kufungwa mabao 2-1 na Ghana katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Machava, jijini Maputo.
 
Kwa mujibu wa Meneja wa Twiga Stars, Furaha Francis hadi mapumziko timu hiyo ilikuwa nyuma kwa bao 1-0. Mwanahamisi Shuruwa aliisawazishia Twiga Stars dakika ya 85, lakini Ghana ikapata bao la pili dakika tatu kabla ya filimbi ya mwisho.
 
Twiga Stars itacheza mechi yake ya pili Septemba 8 mwaka huu dhidi Afrika Kusini. Mechi ya mwisho katika hatua hiyo ya makundi itakuwa Septemba 11 mwaka huu dhidi ya Zimbabwe.

TFF yatangaza mapato ya pambano la Stars

Pambano la mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Algeria (Desert Warriors) limeingiza sh.148,220,000. Mechi hiyo ilichezwa Septemba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mashabiki waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo ni 29,892. Viti vya kijani ambavyo kiingilio kilikuwa sh. 3,000 ndivyo vilivyovutia mashabiki wengi ambapo 17,650 ikiwa ni zaidi ya nusu ya mashabiki wote walinunua tiketi kwa ajili ya viti hivyo.

VIP A ambapo ndipo kulikokuwa na kiingilio cha juu cha sh. 30,000, jumla ya mashabiki 394 walinunua tiketi kwa ajili ya eneo hilo. Viti vya bluu ambapo kiingilio kilikuwa sh. 5,000, mashabiki walionunua tiketi walikuwa ni 8,166.

Viingilio vingine katika pambano hilo vilikuwa sh. 7,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 VIP C na sh. 20,000 VIP B

Sunday, September 4, 2011

TFF yachakachua Ratiba Ligi Kuu

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) jana lilitangaza tena kuipangua ratiba ya mechi za Ligi Kuu ya Tanzania Bara ambayo inaendelea nchini katika viwanja mbalimbali.

Akizungumza jana, Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, alisema kuwa mechi namba 19 kati ya Simba na Villa Squad (zote za Dar es Salaam), iliyopangwa kufanyika Septemba 8, sasa itachezwa Septemba 7 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Wambura alisema vilevile kuwa mechi kati ya Azam na Simba, sasa itachezwa Septemba 10 kwenye Uwanja wa Mkwakwani na hilo limetokana na nia ya kuipa unafuu Azam ambayo itakuwa ikitokea Arusha kucheza dhidi ya JKT Oljoro na kupata fursa ya kumaliza mechi zao kwenye kanda hiyo.

Wambura pia alisema kuwa Kamati ya Mashindano ya TFF imeisogeza mbele kwa siku moja mechi kati ya Coastal Union ya Tanga dhidi ya Moro United ya Dar es Salaam ambapo sasa itachezwa Septemba 8.

Imebainika kuwa ratiba ya awali iliyotolewa na kamati hiyo itakayomalizika Aprili Mosi mwakani itaendelea kupanguliwa kila mara kwani bado haijatoa nafasi kwa timu za Yanga na Simba ambazo mapema mwakani zitashiriki michuano ya Klabu Bingwa Afrika na Kombe la Shirikisho.

Morocco 0 Central African 0



Morocco and Central African Republic stay level on points at the top of Group D, after a 0-0 draw - a result that will be of far more value to the Moroccans, on what could have been tricky trip to Bangui.
The Atlas Lions had plenty of chances in the first half and had a goal disallowed, but the home side managed to keep them at bay and exert their own share of pressure, with both sides drawing a blank in their penultimate qualifying fixture.
The result leaves the group poised for final day drama, with Tanzania and Algeria also still in with contention, after drawing 1-1 on Saturday.
________________________________________________________

Uganda will have to wait until their final Africa Cup of Nations qualifier against neighbours Kenya next month after falling to a 2-0 defeat in Angola.
The result - Uganda's first defeat of the campaign - keeps them at the top of their group, but only by a point from Angola, as the east Africans seek to secure their first appearance at the Nations Cup since 1978.
Elsewhere, Niger leapt to the top of Group G, with a 2-1 victory over South Africa, while Nigeria's vital 2-0 away win in Madagascar was overshadowed by Guinea's 1-0 defeat of Ethiopia, which keeps them three points clear of the Super Eagles.
The BBC's Stephen Fottrell rounds up all the details of the day's action below.
_________________________________________________________
In Group A, Zimbabwe beat Liberia 3-0 in Harare to go second in Group A behind Mali, who defeated Cape Verde 3-0 on Saturday.
Goals from Wilard Katsande, Ovidy Karuru and Khama Billiat secured a convincing victory for the Warriors.
The result takes the group down to the wire on the last day, with Mali away to Liberia and Zimbabwe away to Cape Verde next month.
_________________________________________________________
In Group B, two second-half goals gave Nigeria a valuable 2-0 away win in Madagascar.
The Super Eagles overcame poor playing conditions to claim victory in the last 20 minutes, with goals from skipper Joseph Yobo and a long-range effort from Obinna Nsofor sealing a much-needed win.
The result puts them second in the group behind Guinea, who beat Ethiopia 1-0 to remain top of the table.
Nigeria will now have to beat Guinea by at least two goals on the final day to top the group on the head-to-head rule.
_________________________________________________________
In Group C, Zambia earned a 2-1 victory away to Comoros to put them top of the group and line up a winner-takes-all showdown in Lusaka against Libya in the final round of qualifiers.
The Chipolopolo left it late to take all three points in Moroni, hitting a late winner, having earlier taken the lead through a Christopher Katongo goal, before seeing the Comoros equalise.
Libya beat Mozambique 1-0 on Saturday, in a match played in Cairo because of the civil unrest in Libya, to set up a tight finale to the group.
________________________________________________________
In Group G, Niger secured a massive home victory over South Africa, beating Bafana Bafana 2-1 in Niamey, to put them top of the table.
Dankwa Kofi put the home side ahead in the first half, heading home from a corner, before Mazour doubled their lead from close range.
South Africa pulled one back through Jali but Niger held on for a win that puts them closer to a coveted appearance at the 2012 finals.
With champions Egypt out of contention after losing 2-1 to Sierra Leone on Saturday, the group comes down to a three-way shoot-out for top spot on the final day between Niger, South Africa and the Leone Stars.
________________________________________________________
Burundi grabbed a late equaliser against Benin to share the points in Bujumbura and keep the two teams level on points in Group H.
Papy Faty scored the equaliser for Burundi in the 90th minute, after Guy Akpagba's opener for Benin on 55 minutes.
The result keeps the teams in joint second place in the group, behind Ivory Coast who had already qualified before thumping Rwanda 5-0 on Saturday.
________________________________________________________
Sudan secured a highly valuable 1-0 away win in Congo Brazzaville to bring Group I down to the wire next month.
The result, secured thanks to a second-half goal from Bakri Abdelgadir, puts the Sudanese level on 13 points with Ghana at the top of the group.
The Black Stars beat Swaziland 2-0 on Saturday but will have to wait until October for a winner-takes-all showdown with their fellow group leaders.
________________________________________________________
Uganda began the day in a position to secure their first Nations Cup finals berth in more than 30 years, but will have to wait until their final qualifier against Kenya, after falling to a 2-0 defeat in Angola.
The result - Uganda's first defeat of the campaign - keeps the Cranes top of Group J, but only by a point from Angola.
Kenya are also still in contention, after beating Guinea Bissau 2-1 on Saturday, as the group heads for a fascinating final day climax.
________________________________________________________
Togo earned their first win of the campaign against runaway Group K winners Botswana.
Their 1-0 win, however, matters little as they have no chance of qualifying, whereas Botswana booked their ticket to the finals long before what was their final game of the group.
Malawi still retain the edge in the race towards the automatic second-place qualification spot in the group, after their 0-0 draw with Tunisia on Saturday - a result which leaves them both tied on points, but gives Malawi a superior head-to-head record.

Capello: Lampard inabidi ajipange

Frank Lampard

Kocha wa timu ya Taifa ya Uingereza Mtaliano Fabio Capello, amemuonya Frank Lampard na nyota wote wakongwe wa Uingereza kwamba, wasiwe na uhakika wa namba kwenye kikosi cha wachezaji XI wa kwanza.

Lampard, 33, ambaye ameshacheza jumla ya mechi 87 za Uingereza, aliachwa kwenye benchi mpaka dakika ya 80 alipoingia, wakati Uingereza ikiwa mbele kwa 3-0 dhidi ya Bulgaria, ambapo Capello aliamua kuwaanzisha Scott Parker na Gareth Barry kwenye kiungo cha kati.

Meireles akana Pesa kumuondoa Liverpool

Raul Meireles

Mchezaji wa kimataifa wa Ureno Raul Meireles, amesisitiza kwamba hela si kitu ambacho kilimshawishi kufanya uhamisho wa kushtukiza toka Liverpool na kuhamia Chelsea.

"Haya ni mambo yanayotokea kwenye mpira wa miguu. Nitasema vitu vizuri tu kuhusu Liverpool, nilikuwa na mwaka mmoja mzuri," Meireles aliieleza RTPN.

"Watu wanafikiri mimi ni Yuda na nilihama kwa sababu ya hela. Hiyo haikuwa sababu, nitaelezea wakati mwengine, kwa sasa bado ni mapema.

"Ilitokea haraka sana, mimi si mtu wakulaumiwa kwa kitendo changu cha kuondoka Liverpool, ila sitaacha kuipenda Klabu sababu nina marafiki wazuri sana pale.

"Kitu cha msingi ni kutumia muda wangu wote kuitumikia Chelsea iweze kushinda mataji." Alisema Meireles.

Meireles anategemea kucheza mechi yake ya kwanza akiwa na Chelsea mnamo September 10, wakati timu hiyo inayojulikana maarufu kama The Blues watakapocheza na Sunderland.

Sneijder: Mourinho aliniambia nibaki Inter

Wesley Sneijder

Nyota wa Klabu ya Inter Milan Wesley Sneijder, amefunguka tena na safari hii akisema Kocha wake wa zamani Jose Mourinho, alimwambia awatose Manchester United na aendelee kubaki San Siro.

"Mourinho alinipigia simu akaniambia hivyo. Jamaa ana moyo na timu ya Inter na mara zote amekuwa akinieleza nibaki," Sneijder alilieleza La Gazzetta dello Sport.

"Niko na furaha kwa kubaki hapa, sikuwahi kutaka kuondoka na sitaki kuendelea kuzungumzia kuhusu Manchester United."

"Wakala wangu aliniambia Inter wanataka kuniuza. Tayari nimeongea na Manchester United. Mara ishu juu ya kuuzwa kwa Eto'o ikaanza, hapo mambo yakabadilika," alielezea mchezaji huyo wa kimataifa toka Uholanzi.

Licha ya maelezo yake Sneijder kwamba yuko na furaha hapo Inter, vyombo vya habari nchini Uingereza vimekuwa na taarifa nyingi tofauti vikieleza juu ya uhamisho huu, zaidi ni juu ya uwezekano wa uhamisho huu kufanyika mwezi wa January.

Barcelona: Fabregas Ana Thamani ya £53m

Cesc Fabregas  

Makamu wa Rais wa Klabu ya Barcelona Josep Maria Bartomeu, anaamini kwamba Cesc Fabregas ana thamani ya £53ml, hela ambayo klabu yake ya awali Arsenal ilikuwa inahitaji kuweza kumuuza mchezaji huyo kwa Barca.

Makamu wa Rais huyo amesema, katika kipindi kifupi alichomuona akiitumikia Barcelona na Hispania kwa ujumla, amemkubali sana.

"Baada ya kuona kazi anayoifanya toka awasili hapa, hakika Cesc thamani yake inafika €60ml sawa na £53ml ambazo Arsenal walizihitaji," alisema Bartomeu. "Kijana anacheza kwa kiwango cha juu, na katika kipindi cha wiki tatu ya mazoezi uwezo wake ni wakushangaza . Hakika uhamisho huu ni mzuri, kimasoko hii iko wazi, si yakuficha Cesc ana thamani ya hela nyingi sana.

Wilshere Nje ya Uwanja Mpaka November

Jack Wilshere

Mchezaji Chipukizi Nyota wa Arsenal  Jack Wilshere, ataendelea kuwa nje ya dimba kwa miezi miwili zaidi, hii ni kutokana na kutonesha enka yake ya mguu wa kulia.
Wilshere amekuwa nje ya uwanja kwa kipindi sasa, na hakuwahi kuhusishwa na mechi yoyote ngumu ambayo timu yake ilishiriki toka msimu mpya uanze, na hii ni kutokana na timu hiyo kutotaka kumuwahisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza ambaye kwa sasa anavaa kiatu maalumu kwa ajili ya kuulinda mguu wake, ilikuwa tayari imeshaaminika kwamba mwishoni mwa mwezi July angekuwa umepona, ila  aliutonesha mguu kwenye maandalizi ya msimu, ikiwa ni dakika saba tu toka aingie kwenye mechi dhidi ya New York Red Bulls.
Wilshere, akaja tena kupata maumivu mwezi uliopita akiwa mazoezini, maumivu ambayo yaliaminika yangeweza kumuweka nje ya uwanja kwa wiki mbili au tatu, ila sasa imefahamika atakaa nje ya uwanja mpaka mwezi wa November.
Msemaji wa Klabu ya Arsenal amethibitisha: "Atakuwa nje kwa kipindi cha miezi kadhaa, anahitaji kupumzika, na baada ya hapo tutajua wapi kafikia.''

Sneijder: Uhamisho Man U Unaweza Kamilika January

Wesley Sneijder

Kwa mujibu wa gazeti la Mirror la nchini Uingereza, Wesley Sneijder amewaeleza marafiki zake wa karibu kwamba, uwezekano wa kuhamia Old Trafford unaweza kufanyika mwezi January, licha ya mpango huo kushindikana kwenye kipindi cha usajili kilichomalizika hivi karibuni.
Gazeti hilo limeongeza kwa kuandika, uhamisho wa Sneijder ulishindikana kutokana na mahitaji ya mchezaji huyo wa kimataifa toka Uholanzi kuwa juu sana.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Uingereza mwanzoni walikubali kutoa ada ya uhamisho ya £30m kwa Inter Milan, ila gharama ziliongezeke.
Pamoja na mambo mengine, Sneijder aliwataka United kumkodishia ndege binafsi, na pia kuinunua nyumba yake ya Italy.
Gazeti hili limeeleza kwamba, hapo ndipo Bosi wa United Sir Alex Ferguson alihitaji muda zaidi kufanikisha mahitaji ya kiungo huyo mwanye umri wa miaka 27.
Ila Sneidjer amewaeleza watu wa karibu kwamba uhamishi wake kwenda  Old Trafford unaweza kufufuka mwezi January. Chanzo kimoja kilisema “Wesley alikuwa na nia ya kujiunga United, na makubalianao yalikuwa yanaenda vyema mpaka hatua za mwisho. Walishindwa kuafikina kimipango, ila binafsi yake anasema mwisho wa siku ataishia kuichezea Manchester United.” 

Saturday, September 3, 2011

Kolo Toure Ndani, Hargreaves Nje Kikosi Cha Man City .

Kolo Toure

Klabu ya Manchester City, imetaja kikosi cha wachezaji 23 watakaoshiriki kwenye mashindano ya Kombe la Mabingwa Barani Ulaya, huku kiungo aliyesajiliwa hivi karibuni Owen Hargreaves akienguliwa kwenye kikosi hicho.

Kiungo huyo ameshindwa kujumuishwa kwenye kwenye kikosi cha wachezaji 23 wa Roberto Mancini licha ya hivi karibuni kusajiliwa na timu hiyo.

Beki Kolo Toure amejumuishwa kwenye kikosi baada ya kuwa nje ya Uwanja kwa Miezi sita kutokana na kesi iliyokuwa inamkabili ya kutumia madawa.

 Mchezaji mwingine wa timu hiyo Wayne Bridge, ametoswa kwenye kikosi japo haikuelezwa sababu ya kuachwa kwake.

Kikosi Kamili cha Man City Ligi ya Mabingwa :

Makipa: Joe Hart, Costel Pantilimon, Stuart Taylor.

 Mabeki: Gael Clichy, Joleon Lescott, Nedum Onuoha, Micah Richards, Aleksandar Kolarov, Vincent Kompany, Kolo Toure, Pablo Zabaleta, Stefan Savic.

Viungo: Gareth Barry, Adam Johnson, James Milner, Nigel De Jong, Samir Nasri, David Silva, Yaya Toure.

Washambuliaji: Sergio Aguero, Edin Dzeko, Carlos Tevez, Mario Balotelli.

Senegal book place in finals


Senegal secured their place in next year's African Nations Cup with a 2-0 win over DR Congo.
Moussa Sow put Senegal in front in the 35th minute and, although they had a second ruled out for offside before half-time, Sow found the net again in the 52nd minute to secure the points and lock-up qualification.
Senegal join Botswana and Ivory Coast in qualifying for the tournament, while co-hosts Equatorial Guinea and Gabon also have places secured.
Victory for Senegal leaves Cameroon facing an uphill battle to qualify, and they were largely unimpressive against lowly Mauritius before somehow compiling a flattering 5-0 scoreline.
Goals from Leo Kweuke and Matthew Andongcho put them in charge before Samuel Eto'o added a third from the penalty spot.
A late brace from Eric Choupo-Moting gave the Indomitable Lions a margin of victory they scarcely deserved, even before Eyong Enoh's late goal was disallowed for handball.
Defending champions Egypt had their elimination confirmed as a youthful side went down 2-1 to Sierra Leone.
Sheriff Suma got the opening goal in the 14th minute and, although Mohsen Maruwen equalised on the stroke of half-time, Mohamed Bangura's late penalty ended Egypt's campaign.
Sierra Leone move level with South Africa at the top of Group G ahead of the latter's clash with Niger on Sunday.
There was no place for Kolo Toure - eligible again after completing a six-month drugs ban - in the Ivory Coast starting line-up but they did not miss him in a 5-0 demolition of Rwanda in Group H.
The Ivory Coast goals came in a flood, with Salomon Kalou's opener swiftly followed by a quickfire brace from Wilfried Bony that left Rwanda reeling in Kigali.
In the second half, Gervinho teed up Didier Ya Konan for the fourth before getting the fifth himself as the Elephants, who have already qualified, ran riot.
Libya, playing in Egypt under the nation's new flag and in a new kit after the fall of Muammar Gaddafi, recorded a 1-0 win over Mozambique thanks to Reyad Ellafi's 31st-minute goal, sending them top of Group C ahead of Zambia's game against Comores on Sunday.
A goal in the dying minutes from Tangeni Shipahu gave Namibia a 1-0 win over the Gambia, which sees them draw level with their opponents in Group F but effectively hand Burkino Faso qualification as they sit five points clear at the top.
Denis Oliech's late goal gave Kenya a vital 2-1 win over Guinea Bissau in Nairobi.
Needing victory to keep their hopes alive, Kenya had to wait until the hour mark to see Mike Baraza break the deadlock, and then watched as Danilo Luis Pereira lashed home an equaliser in the 89th minute.
But just as hope was fading, Oliech scored in the 92nd minute for secure three points that keep Kenya's qualification hopes alive in Group J.
Uganda can qualify from the group on Sunday with a victory over Angola, who would then face a battle with Kenya for second place.
Cheick Diabate's quick brace put Mali on course for a 3-0 victory over Cape Verde that sent them to the top of Group A. Mahamand Traore made sure of the win in the second half.

In Group D, Tanzania and Algeria did little to help their qualification hopes with a 1-1 draw.
Tanzania took the lead through Mbwana Samata midway through the first half, but Hameur Bouazza fired in an equaliser just before the hour mark, leaving both teams on five points, trailing Morocco and Central African Republic - who clash on Sunday - by two points.
In Group K, Malawi and Tunisia drew 0-0, leaving both teams locked on 11 points in the battle for second place behind Botswana.

Gerrard kurudi dimbani Sept. 18

Steven Gerrard

Mchezaji wa timu ya Liverpool Steven Gerrard, yuko karibu kurudi uwanjani baada ya kuwa nje ya dimba kwa kipindi cha miezi mitano kutokana na majeraha yaliyokuwa yanamkabili.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, ameshindwa kuichezea timu Liverpool na timu ya Taifa ya Uingereza toka mwezi wa March kutokana na upasuaji uliofanywa kwenye goti lake.

Anategemea kurudi kwenye mechi ya Ligi kuu ya Uingreza siku ambayo timu yake itakabiliana na Tottenham.

Gerrard ameueleza mtandao Liverpool "Najisikia vizuri sana, nimerudi na kwa sasa naweza hata kupiga mpira, naona mambo sasa yapo sawa. Naamini nitarudi kamili mazoezini siku ya Alhamisi ua Ijumaa."

Gerrard aliongeza: "Sitokuwepo kwenye mechi dhidi ya Stoke Jumamosi ijayo, ila naamini nitahusishwa moja kwa moja kwenye mechi yetu dhidi ya Tottenham, ila bado utabaki kuwa uwamuzi wa Kenny kama naweza kurudi uwanjani ."

"Nimekuwa na mapumziko marefu, nina nguvu na ari tena, najua nitarudi nikiwa fiti, mwenye nguvu na mwenye uchu wa hali ya juu ambao sijawahi kuwa nao". Alisema Gerrard.

Friday, September 2, 2011

Taifa Stars Lazma Kieleweke LEO


Kikosi Cha Stars

KIKOSI cha Taifa Stars kinaingia leo uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kupambana na Algeria katika mechi ya kuwania kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika.

Hii ni mechi ya marudiano kwa timu hizi kwa sababu katika mechi ya kwanza iliyofanyika kwenye uwanja wa Mustafa Tchaker uliopo mjini Blida kilomita 45 kutoka katika mji wa Algiers, Taifa Stars ilitoka sare1-1.

Mpaka sasa kikosi cha Taifa Stars kimepoteza mechi mbili katika mechi nne kilichocheza katika kutafuta nafasi ya kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika 2012 zitakazofanyika kwenye nchi za Gabon na Guinea ya Ikweta.

Mechi ya mwisho Taifa Stars ilishindwa kutamba mbele ya timu ya Jamhuri ya Afrika ya Kati baada ya kuchapwa mabao 2-1 kwenye uwanja wa Barthelemy Boganda mjini Bangui.

Kutokana na kupoteza mechi hiyo Taifa Stars hivi hivi sasa ipo katika nafasi ngumu ya kufuzu kushiriki fainali hizo za Afrika, ambapo imebakisha mechi mbili ambazo inatakiwa kushinda mechi zote ili ifikishe pointi 10 kuweza kufuzu.

Taifa Stars imebakisha mechi dhidi ya Algeria ambayo inachezwa leo jijini Dar es Salaam, pia imebakisha mechi dhidi ya Morocco ambayo itachezwa huko mjini Rabat kwenye uwanja wa Prince Moulay Abdellah kati ya tarehe 7,8,9/10/2011.

Mpaka sasa Taifa Stars imeshinda mechi moja ambayo iliifunga Jamhuri ya Afrika ya Kati mabao 2-1 katika pambano lililopigwa jijini Dar es Salaam, ilitoka sare ya bao 1-1 na Algeria, vile vile Stars ilifungwa bao 1-0 na Morocco kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kwa mechi ilizocheza Taifa Stars hivi sasa inashika nafasi ya tatu katika kundi D ikiwa na pointi nne sawa na Algeria inayoshika nafasi ya nne ikiwa na pointi nne, timu inayoshika nafasi ya kwanza katika kundi hilo ni Morocco yenye pointi saba ikifuatiwa na Jamhuri ya Afrika ya Kati ambayo ina pointi saba pia.

Morocco yenyewe hivi sasa imebakisha mechi dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati mechi itakayochezwa mjini Bangui pia imebakisha mechi dhidi ya Tanzania itakayochezwa mjini Rabat, wakati Jamhuri ya Afrika ya Kati imebakisha mechi dhidi ya Morocco mjini Bangui na mechi dhidi ya Algeria huko nchini Algeria.

Algeria pia imebakisha mechi ya leo dhidi ya Tanzania mjini Dar es Salaam na mechi dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati huko nchini Algeria.

Kama Morocco ikishinda mechi zote itafikisha pointi 13 na Jamhuri ya Afrika ya Kati ikishinda mechi zote itafikisha pointi 13 , hivyo Taifa Stars ina kazi kubwa ya kufanya, vile vile inatakiwa kuomba Morocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati zifanye vibaya katika mechi zilizobakia.

Ni wazi wachezaji wetu waliochaguliwa na kocha Poulsen kuunda kikosi cha timu ya taifa hivi sasa wana kazi kubwa ya kulivusha taifa la Tanzania katika kipindi hiki kigumu ili tuweze kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika 2012.

Wachezaji wa Stars leo wanatakiwa kuingia uwanjani wakiwa na lengo moja tu la kupata ushindi siyo kutoka sare wala kufungwa.

Tunafahamu mchezaji wa timu ya taifa kazi yake ni kupigania kitu ambacho huwa na thamani na kumbukumbu kubwa kwa vizazi vingi vitakavyofuatia.

Kitu wanacholeta wachezaji wa timu ya taifa ni ushindi, siku zote wachezaji wa timu ya taifa wanaposhinda huwa wanaliletea taifa lao furaha na kujisikia fahari kuishi katika taifa hilo, hivyo tunatarajia wachezaji waliochaguliwa na kocha Jan Poulsen wataweza kutuletea furaha wananchi wa Tanzania katika mechi ya leo.

Tunaamini wachezaji wa Stars watatumia akili ya mchezo kwa ahali ya juu, nguvu na stamina waliyonayo ili kupata ushindi leo.

UEFA Euro 2012 Qualifying Results

Rooney & Terry

Group A

Germany remain perfect in their qualifying campaign (8 for icon cool UEFA Euro 2012 Qualifying Results with a very comfortable win over Austria, 6-2, at Gelsenkirchen. Mesut Ozil scored a hat trick, with Lukas Podolski, Andre Schurrle and Mario Gotze doing the rest. The Germans were up 3-0 in less than 28 minutes, but a goal from Marko Arnautovic cooled them off for a short while. Martin Harnik scored the second for Austria.
Turkey beat Kazakhstan 2-1 with a deep deep injury time goal by Arda Turan. Belgium were held to a costly 1-1 draw at Baku against Azerbaijan. 
Gemrnay, with 24 points after 8 matches, are clear and set in the 2012 Euros. Turkey are second with 13 points after seven games played, Belgium are third with 12 points and eight games played. Both still have to face the Germans.

Group B

Still very tight in the group – Ireland were held at home to a 0-0 draw against Slovakia, Armenia beat Andorra 3-0 in Andorra while Russia squeezed out a 1-0 win over Macedonia in Moscow with a goal from Igor Semshov, the 33 year old from Dynamo Moscow.
All nations have played 7 matches – Russia lead the group with 16 points, Ireland and Slovakia with 14 and Armenia still in the mix with 11 points. Ireland play in Moscow on Tuesday while Armenia visit Slovakia.

Group C

Italy nearly secure their place in the tournament with a 1-0 win in the Faroe Islands with an early Antonio Cassano goal. Estonia stunned Slovenia in Ljubljana with goals from Konstantin Vassilijev and Ats Purje. Serbia earned a crucial 1-0 win over Northern Ireland through Marko Pantelic.
Italy lead the group with 19 points, but it’s all tight from there – Slovenia (8 matches) have 11 points, Serbia have 11 but a game less, Estonia (8) have 10 points and Northern Ireland (7) have 9 points.

Group D

France remain in control of the group with a 2-1 win in Tirana against Albania with goals from Karim Benzema (his 13th goal for France and 3rd in these qualifiers) and Yann M’Vila. Bosnia won 2-0 in Belarus with goals from Sejad Salihovic and Haris Medunjanin. Romaina grabbed a 2-0 victory against Luxemborg with two goals from Gabriel Torje (Udinese).
France lead the group with 13 points in six matches. Bosnia have 13 in 7, Belarus have 12 in 8 and Romania have 11 in 7.

Group E

The Netherlands didn’t hold back against amateurish (at best) San Marino winning 11-0, remaining perfect on their easy road towards Poland and the Ukraine. Robin van Persie forgot his Arsenal woes, scoring four goals, making it six for him in these qualifiers. Wesley Sneijder and Klaas Jan Huntelaar scored two each. Hungary got a huge win over Sweden through a 90th minute goal from Gergely Rudolf, getting the 2-1 win. Finalnd beat Moldova 4-1.
The Dutch have 21 points in 7 matches. Sweden have 15 from 7 while Hungary have 15 from 8. Sweden still have to play the Dutch again (in Sweden), but they do win the tie breaker with Hungary thanks to their 2-0 win at home.

Group F

Greece got a big win in Israel, 1-0 through Sotiris Ninis, leaving Israel hardly a chance to qualify from the group. Croatia got a 3-1 win in Malta and Latvia beat Georgia 1-0. Greece have 17 points after 7 matches, Croatia are with 16 at second. The Greeks host Croatia next month.

Group G

England remained perfect away from Wembley, beating Bulgaria 3-0 with goals from Gary Cahill and Wayne Rooney (2), reaching 28 for the national team. Wales did England a huge favor with their first win of the qualifiers, beating Montenegro 2-1 in Cardiff through Steve Morison and Aaron Ramsey.
England lead the group with 14 points after six matches, Montenegro are second with 11.

Group H

Things are still rather complicated in this one, with three nations in the picture. Group leaders Portugal won 4-0 in Cyprus, with Cristiano Ronaldo scoring twice, taking him to 29 international goals and four in these qualifiers. Norway got a late penalty to give them a 1-0 win over Iceland, scored by Mohammed Abdellaoue. 
Portugal have 13 points at first, same as Norway. Both teams beat each other 1-0 in their home matches. Denmark are third with 10 points and 5 matches. They host Norway on Tuesday and host Portugal next month.

Group I

Only one match played today – Lithuania drew Lichtenstein without any goals. Spain lead the group with 15 points (100%), the Czech Republic, playing in Scotland tomorrow, are second with 9 points. Scotland have only 4 points at fourth after four matches, and can’t afford not to win at Hampden Park tomorrow if they want to have a chance of finishing second.

Ujerumani ya Kwanza Kutinga UEFA EURO 2012


Wachezaji wa Ujerumani Wakipongezana

Germany 6 vs 2 Austria
Ujerumani imekuwa nchi ya kwanza kufaulu kuingia kwenye Fainali za UEFA EURO 2012, na hii ni baaada ya ushindi wa mabao 6-2 dhidi ya Austria.

Magoli ya Ujerumani yalifungwa na  8′ Miroslav Klose, 23′ Mesut Özil, 28′ Lukas Podolski,  47′ Mesut Özil,   84′ Andre Schürrle na 89′ Mario Götze. Wakati yale ya Austria yalifungwa na  
 Marko Arnautovic 42′ na Martin Harnik 51′

Chicharito Asawazisha Poland vs Mexico

Javier 'Chicharito' Hernandez

Mchezaji wa timu ya Manchester United, Javier 'Chicharito' Hernandez, amerejea tena uwanjani kuichezea timu ya Taifa lake la Mexico, na kuweza kuisaida kutoka sare1-1 dhidi ya Poland,

Chicharito aliweza kuisaidia timu hiyo, baada ya kufunga goli la kusawazisha lililopelekea mechi hiyo kuisha kwa sare.

Hii ilikuwa ni mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye uwanja wa Pepsi Arena kwenye jiji la Warsaw

Uholanzi yafanya Mauwaji

Wachezaji wa Uholanzi Wakipongezana

Timu ya taifa ya Uholanzi imejiwekea rekodi yake ya ushindi mkubwa zaidi kuwahi kupata, hii ni baada ya kuifunga San Marino kwa mabao 11-0

Kwa ushindi huo, Uholanzi imeendelea kujiweka kwenye mazingira mazuri ya mbio za kusaka tiketi ya kushiriki Kombe la Mataifa ya Ulaya hapo mwakani.

Magoli yaliyofungwa na Robin van Persie (4x), Wesley Sneijder (2x), John Heitinga, Klaas-Jan Huntelaar (2x) Dirk Kuyt na Georginio Wijnaldum, yalisaidia kuiwapa vijana hao wa Oranje pointi tatu, kwenye mechi iliyochezwa ndani ya jiji la Eindhoven.

Kufuatia ushindi huu, Uholanzi sasa wamefikisha jumla ya pointi 21 kutokana na michezo saba walizocheza, huku wakiwa nanaongoza Kundi E la Michuano hiyo, na mechi inayofuata watacheza September 6 dhidi ya Finland.

San Marino wanaendelea kukamata mkia kwenye kundi hilo, wakiwa hawana poiti hata moja kwa mechi nane walizocheza, na watakutana na Sweden kwenye mechi itakayofata ikichezwa Jumanne ijayo.


 7′ Robin Van Persie   12′ Wesley Sneijder   17′ John Heitinga   49′ Dirk Kuyt   56′ Klaas-Jan Huntelaar   65′ Robin Van Persie   67′ Robin Van Persie   77′ Klaas-Jan Huntelaar   79′ Robin Van Persie   87′ Wesley Sneijder   90′ Georginio Wijnaldum

Fergie na Dzeko Watwaa Tuzo za Mwezi Barclays


Sir Alex Ferguson

Kocha wa timu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson, ametangazwa kuwa Meneja wa mwezi Barclays Premier League kwa mwezi wa nane, hii ikiwa ni mara ya 26 kwake kushinda tuzo.

Na kwa upande mwingine Mshambuliaji wa Manchester City Edin Dzeko, amechaguliwa mchezaji bora wa mwezi wa August na kushinda Tuzo hiyo upande wa wachezaji .

Mchezaji Mpya wa Arsenal Mkorea Park Chu-Young apiga Hat-Trick

Park Chu-Young

Mchezaji mpya wa Arsenal Park Chu-Young, mchana wa leo ameiwezesha Nchi yake Korea Kusini kupata ushindi a magoli 6-0 dhidi ya Lebano.

Katika mchezo Park Chu-Young aliweza kufunga magoli matatu (hat-trick), huku magoli mengine yakifungwa na mshambuliaji mpya wa timu ya Sunderland Ji Dong-Won, huku mengine mawili yakifungwa na kiungo wa Timu ya Sangju Sangmu  Kim Jung-Woo.

Kwa ushindi huo Korea Kusini, imejiweka kwenye mwanzo mzuri wa kampeni yake, kuweza kupata tiketi ya kushiriki kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

Bendtner: Sirudi Tena Arsenal


Nicklas Bendtner

MUDA mchache baada ya kufanikisha uhamisho wake wa mkopo na kujiunga na Klabu ya Sunderland , mshambuliaji wa Arseanl Nicklas Bendtner amesema hatorudi tena kwenye klabu hiyo ya Emirates.

Kwa kipindi cha miaka sita alichokuwa timu hiyo Bendtner, 23, ameonekana kuwagawa kimawazo mashabiki wengi wa Arsenal, kuna ambao wanaamini ana uwezo na anahitaji kufanikiwa kwa kiwango cha juu na kuna wale wanaomuona sio.

Mchezaji huyo wa kimataifa toka Denmark anaamini alistahili kuwa anaongoza safu ya ushambuliaji wa timu hiyo, ila mwisho wa siku imekuwa ni kinyume kwa kocha wake Arsene Wenger.

Msimu uliopita Bendtner, alipata nafasi chache za kucheza kwenye kikosi cha timu hiyo na hasa baada ya kupata ajali ya gari miaka miwili iliyopita, na sasa amejiunga na Klabu ya Sunderland kwa mkopo.

Nyota Stars: Hakika Kitaeleweka


Nizar Khalfan

Wachezaji Nyota wa Tanzania wanaokipiga nje ya nchi wamewataka mashabiki na wadau wote wa soka kujitokeza kwa wingi kesho kwenye Uwanja wa Taifa na kuwapa sapoti ya kutosha kwani wamekuja kivingine na kuahidi ushindi mkubwa dhidi ya Algeria.

Nyota hao saba ni Nizar Khalfan (Vancouver WhiteCaps, Canada), Danny Mrwanda na Abdi Kassim (Don Long, Vietnam), Mbwana Samata (TP Mazembe, DR Congo), Henry Joseph, Athuman Machupa na Idrissa Rajabu (Sofapaka, Kenya).

Pambano hilo la kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Mataifa ya Afrika nchini Gabon na Guinea ya Ikweta mwakani litapigwa kesho jioni kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti baadhi ya nyota hao jana walisema uwezo wa Tanzania kuifunga Algeria upo kulingana na mchezo wa awali waliocheza nayo mjini Algers, ambapo mchezo huo ulimalizika kwa sare ya bao 1-1. 

 
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika mjini Algers mwezi Machi mwaka huu Taifa Stars iliilazimisha sare ya 1-1 Algeria ikiwa ugenini.

Cheka Amtwanga Maugo kwa Pointi

Cheka na Maugo Ulingoni

BONDIA Francis Cheka ‘SMG’ kutoka Morogoro, alimdunda bondia Mada Maugo ‘Mbunge wa Musoma’ katika pambano lisilo la kuwania ubingwa, lililofanyika Mjini Morogoro kwenye uwanja wa Jamuhuri.

Maugo ambaye kabla ya pambano hilo alikuwa akijidadi kuwa atampiga vibaya Cheka kwa kipigo cha mbwa mwizi, alishindwa kutimiza kauli hiyo na badala yake yeye ndie alikumbana na wakati mgumu ulingoni.

Pambano hilo lisilokuwa la ubingwa, lilichezeshwa na waamuzi toka chama cha TPBC ambapo, Jaji wa kwanza alitoa matokeo ya sare kwa mabondia wote yaani  alama 98-98, wakati Jaji wa pili alimpa Cheka ushindi wa alama 99-98, na Jaji wa tatu alimpa Cheka ushindi wa alama 100-98.

Milan Wamtema Inzaghi Kwenye Kikosi Cha Ligi Ya Mabingwa Ulaya


Filippo Inzaghi

Mshambuliaji mkongwe wa timu ya AC Milan Filippo Inzaghi, ametemwa kwenye kikosi cha AC Milan kitakachoshiriki kwenye Ligi Ya Mabingwa Barani Ulaya msimu huu, hii inamfanya Inzaghi ashindwe kuvunja rekodi ya ufungaji wa mabao inayoshikiliwa na Raul kwa sasa.

Akiwa amecheza mechi 115 na kufunga magoli 70, Inzaghi anaendelea kuwa nyuma ya Raul ambaye mpaka sasa amemtangulia kwa magoli mawili zaidi, Raul ambaye ni mmoja kati ya wachezaji wanaoheshimika na Real Madrid, ana jumla ya magoli 72 katika michuano hiyo.

Na kwa umri wa miaka 38 alionao Inzaghi, inaonyesha moja kwa moja mchezaji huyo tamati yake ndio imefika, na itakuwa ngumu kuweza kulinyakua tena taji ambalo Raul alilipora kwake msimu uliopita.

Msimu uliopita kwenye ligi hiyo Raul alifunga magoli matano akiwa na timu ya Schalke ya nchini Ujerumani, na kuweza kumpiku gwiji huyo aliyekuwa anaongoza kwa kipindi kirefu.

Neville: Uingereza Isingechukua Kombe La Dunia Hata Ferguson Angekuwa Kocha



Mchezaji wa zamani wa Manchester United na Timu ya Taifa ya Uingereza Gary Neville, amesema timu ya Taifa ya Uingereza isingeweza kutwaa kombe la Dunia mwaka 2010 hata kama Sir Alex Ferguson angekuwa kocha.
Timu ya Taifa ya Uingereza ilitolewa kwenye hatua ya pili ya mashindano hayo yaliyofanyika Afrika Ya Kusini, huku Neville akiendelea kusema kwamba, timu imekosa umoja, nguvu na vipaji halisi toka kwa wachezaji, kitu ambacho kinapelekea kushindwa kufanya vizuri.

Leo timu hiyo leo inaingia uwanjani kucheza na timu ya Taifa ya Bulgaria, kuwania nafasi ya kushiriki michuano ya Bara la Ulaya, mchezo utakaopigwa kwenye uwanja wa Vasil Levski Stadium, Sofia, kuanzia saa Moja na Robo kwa saa za UK.

Thursday, September 1, 2011

Tevez Anaweza Endelea Kubaki City

Tevez & Aguero

Mshambuliaji wa Manchester City Carlos Tevez, " kwa sasa yupo na furaha kwenye Klabu yake", na kuna uwezekano mkubwa wa kuendelea kubaki na kuitumikia timu hiyo ya Eastlands kwa kipindi kirefu, hii ni kwa mujibu wa muwakilishi wake Kia Joorabchian.

Ujio wa Mke na Watoto wake ndani ya Manchester hivi karibuni, umefuta matamanio ya kutaka kuihama klabu hiyo, na kuna kila sababu za yeye kuweza kubaki, alisema Kia Joorabchian. Na hata uwepo wa mchezaji mwenzake toka nchi yake ya Argentina Sergio Aguero, zinapelekea moja kwa moja kumshawaishi Tevez kubaki Manchester City.

Kikosi Cha Wachezaji XI Waliosajiliwa EPL

Dirisha la Usajili limefungwa rasmi jana saa 5 Usiku kwa saa za Uingereza, na litafunguliwa tena mwezi January likifahamika kama dirisha Dogo. Kwa mtazamo wake, Mchambuzi wa BBC Sports Mark Lawrenson ametaja listi ya wachezaji 11, na hawa ni wachezaji waliosajiliwa katika kipindi cha usajili toka vilabu vya nje ya Uingereza, na hii hapa ndio Starting XI yake.


Upi Mtazamo wako?
Toa maoni yako kwa kubofya hapo chini palipoandikwa comments