Monday, September 5, 2011

Santos: Hakuna makubaliano ya kuuzwa Neymer

Neymar

Klabu ya Santos  ya nchini Brazil imesema haijafikia makubaliano na timu yoyote juu ya uwezekano wa kumuuza mshambuliaji wake Neymar.

Klabu hiyo imetoa tamko hilo Jumapili kwenye taarifa ndefu waliyoitoa kwenye Mtandao wake, taarifa hiyo imesisitiza kwamba, hakuna dili yoyote ambayo wamefikia na Barcelona juu ya kumuhamisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19, kwenda Camp Nou ifikapo mwaka 2013.

"Kutokana na sababu binafsi zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari hivi karibuni kuhusiana na Neymar, Santos Futebol Clube inapenda kutoa tamko rasmi kwamba, maelezo yanayotolewa na vyombo hivyo juu ya mustakabali wa Neymer sio za kweli” taarifa hiyo ilisema.

"Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu mara zote imekuwa na nia njema ya kuendelea kubaki na Neymer kwenye timu.”

Taarifa hiyo imekuja baada ya gazeti la Estadao siku ya Jumamosi kuandika kwamba, Santos na Barcelona wamefikia makubaliano ya awali kwa Neymar kujiunga na mabingwa Hispania na Ulaya baada ya miaka miwili toka sasa.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Bazil amekuwa akihusishwa na kuhamia Barcelona na pia kwa mahasimu wao Real Madrid katika kipindi cha majira ya joto, huku baadhi ya timu nyingine za Bara la Ulaya zikihusishwa juu ya mpango huo, ila mchezaji juyo amekuwa akisisitiza kwamba kwa muda huu angependa kuendelea kucheza nchini mwake.

No comments:

Post a Comment