Wednesday, August 31, 2011

Dirisha la Usajili Ulaya Lafungwa

Mikel Arteta - Everton to Arsenal, undisclosed
Craig Bellamy - Manchester City to Liverpool, undisclosed
Peter Crouch - Tottenham to Stoke, undisclosed
Raul Meireles - Liverpool to Chelsea, undisclosed
Shaun Wright-Phillips - Manchester to QPR, undisclosed
Wilson Palacios - Tottenham to Stoke City, undisclosed
Alan Hutton - Tottenham to Aston Villa, undisclosed
Jermaine Jenas - Tottenham to Aston Villa, season loan
Yossi Benayoun - Chelsea to Arsenal, season loan
Cameron Jerome - Birmingham to Stoke City, undisclosed
Scott Dann - Birmingham to Blackburn, undisclosed
Per Mertesacker - Werder Bremen to Arsenal, undisclosed
Owen Hargreaves - Manchester City, free
Scott Parker - West Ham to Tottenham, undisclosed
Andre Santos - Fenerbahce to Arsenal, undisclosed
Joe Cole - Liverpool to Lille, season loan
Christian Poulson - Liverpool to Evian, undisclosed
David N'gog - Liverpool to Bolton, undisclosed
Gael Kakuta - Chelsea to Bolton, five-month loan
Shaun Maloney - Celtic to Wigan, undisclosed
Brian Ruiz - FC Twente to Fulham, undisclosed
Orlando Sa - Porto to Fulham, undisclosed
Anton Ferdinand - Sunderland to QPR, undisclosed
Royston Drenthe - Real Madrid to Everton, season loan
Denis Stracqualursi - Tigres to Everton, season loan
Darnel Situ - Lens to Swansea, £250,000
Badr El Kaddouri - Dynamo Kiev to Celtic, five-month loan
Pablo Ibanez - West Brom to Birmingham, undisclosed
Fede Bessone - Leeds to Swansea, free
Zdenek Grygera - Juventus to Fulham, free transfer
Tommaso Trani - Milan to QPR, free agent
Henri Lansbury - Arsenal to West Ham, season loan
Guy Demel - Hamburg to West Ham, free
Liam Feeney - Bournemouth to Millwall, undisclosed
Patrick van Aaanholt - Chelsea to Wigan, season loan
John Guidetti - Manchester City to Feyenoord, season loan
Enda Stevens - Shamrock Rovers to Aston Villa, from Jan 2012
Villyan Bijev - California Odyssey to Liverpool, undisclosed
James Hurst - West Brom to Blackpool, season loan
Daniel Bogdanovic - Sheffield United to Blackpool, undisclosed
Joe Garner - Nottingham Forest to Watford, undisclosed
Dany N'Guessan - Leicester to Millwall, undisclosed
Ben Turner - Coventry City to Cardiff City, undisclosed
Alassane N'Diaye, Crystal Palace, released
Mark Beevers - Sheff Wed to MK Dons, four-month loan
Giles Coke - Sheff Wed to Bury, two-month loan
Anthony McNamee - Norwich to MK Dons, free
Callum Tapping - Tottenham to Hearts, undisclosed
Kelvin Langmead - Peterborough to Northampton, five-month loan
Keammar Daley - Tivoli Gardens to Preston, undisclosed
Tom Adeyemi - Norwich City to Oldham, five-month loan
Ahmed Abdulla, West Ham to Swindon Town, six-month loan
Jed Wallace - Lewes to Portsmouth, undisclosed
Michael Smith - Darlington to Charlton, undisclosed
Emile Sinclair - Macclesfield to Peterborough, undisclosed
Max Gradel - Leeds to St Etienne, undisclosed
Mike Grella - Leeds to Brentford, undisclosed
Peter Ramage - QPR to Crystal Palace, five-month loan
Ryan McGivern - Man City to Bristol City, season loan
Matt Duke - Bradford, free
Jay Simpson - Hull to Millwall, four-month loan
Martyn Waghorn - Leicester to Hull, four-month loan
Michael Timlin - Swindon to Southend, four-month loan
Brett Williams - Reading to Rotherham, five-month loan
Simon King - Gillingham to Plymouth, one-month loan
Damien Mozika - Bury to Scunthorpe, undisclosed
Shaun Harrad - Northampton to Bury, undisclosed
Jamie Griffiths - Ipswich to Plymouth, one-month loan
Andrew Little - Rangers to Port Vale, five-month loan
Jamie Devitt - Hull to Bradford, five-month loan
Shane Byrne - Leicester to Bury, one-month loan
Tom Collins - Stevenage to Hayes and Yeading, one-month loan
Mitchell Nelson - Bournemouth to Lincoln, one-month loan
Peter Winn - Stevenage to Cambridge United, three-month loan
Terry Dixon - Bradford City to Halifax, one-month loan
Ben Swallow - Bristol Rovers to Bath City, three-month loan
John Fleck - Rangers to Sheffield United, season loan
Kyle Hutton - Rangers to Sheffield United, season loan
Mohamadou Sissoko - Udinese to Kilmarnock, season loan
Jude Winchester - Linfield to Kilmarnock, undisclosed
Michael Paton - Aberdeen to Stockport, four-month loan
Ross McKinnon - Motherwell to Dumbarton, one-month loan
Steven Howarth - Motherwell to Alloa, one-month loan
Ryan Connolly - Derby to Ayr, three-month loan

Raul Meireles wa Liverpool ahamia Chelsea

Raul Meireles

Kiungo wa Liverpool Raul Meireles, amefanya uhamisho wa aina yake na kujiunga Chelsea kwa thamani ya £12m.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, alituma maombi ya kuhama Anfield muda mfupi kabla ya dirisha la usajili halijafungwa, na ameweza kuingia mkataba wa miaka minne na watoto wa darajani.

Meneja wa Chelsea Andre Villas-Boas aliwahi kufanya kazi sambamba na mchezaji huyo walipokuwa Porto kabla ya mchezaji huyo kuelekea Anfield mnamo mwezi August mwaka jana.

Meireles kwa sasa ni majeruhi, baada ya kuumia kwenye mechi ya Liverpool ilipocheza na Exeter City kwenye kombe la Carling mapema wiki iliyopita.

Mwanzoni Liverpool waliikataa ofa ya Chelsea kwa mchezaji huyo, ambapo walikuwa wapo tayari kutoa £8m sambamba na Yossi Benayoun ili kuweza kumpata.

Arsenal Yawasajili Mikel Arteta, Yossi Benayoun na Per Mertesacker


Mikel Arteta

Klabu ya Arsenal imemsajili beki wa Everton Mikel Arteta kwa kiasi cha £10m,  hii ni baada ya mchezaji huyo kutuma maombi ya kuhama.

Kiungo huyo wa ki-spania amejiunga na washika bunduki hao kwa mkataba wa miaka minne, na hiyo ilitokea muda mfupi kabla ya dirisha la usajili kufungwa saa tano kamili kwa saa za Uingereza.

Arsenal pia imefanikiwa kumpata kwa mkopo mchezaji wa Chelsea Yossi Benayoun, kwa msimu mmoja.

Benayoun, ambaye ni nahodha wa nchi yake ya Israel, ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter akisema "Nimesajili na Arsenal, nina furaha sana na kupendezwa na jambo hili, ila kwa sasa kichwa changu kinafikiria juu ya mechi dhidi ya Ugiriki hapo Ijumaa, asanteni kwa ushirikiano wenu."

Klabu zote mbili zimethibitisha juu ya maafikiano hayo.

Pia imefahamika kwamba Arsenal wamekamilisha usajili wa Beki wa kimataifa wa Ujerumani Per Mertesacker toka Werder Bremen.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, inaaminika amewagarimu washika bunduki wa Emirates kiasi cha  £8m huku akiwa amesaini mkataba wa muda mrefu.

"Nilikuwa na wakati mzuri na Werder, hakika nawaheshimu sana, ila kuhamia London ni kama ndoto iliyokuwa kweli," alisema Mertesacker huku akiongeza "Kwangu mimi English Premier League mara zote naiona ina mvuto ikiwa na ushindani wa hali ya juu"

Meneja wa timu hiyo Arsene Wenger aliieleza kwenye mtandao wa timu hiyo: "Tumefurahi kumkaribisha Per Mertesacker kwenye Klabu yetu."

Bellamy Arejea Liverpool

Craig Bellamy

Klabu ya Liverpool imethibitisha kumsajili mchezaji aliyewahi kuichezea timu hiyo Craig Bellamy.



Mchezaji huyo ambaye ni nahodha wa Wales, amerudi tena Anfield kwa mkataba wa miaka miwili baada kuwa huru toka Manchester City.

Bellamy ambaye aliondoka Liverpool baada ya msimu wa 2007 na kujiunga na West Ham, inaaminika atasaidia kuongeza nguvu ya ushambuliaji kwenye kikosi cha Kenny Dalglish, akiwa mchezaji wa ziada nyuma ya Luis Suarezna Andy Carroll.

Mbwana Samatta: TP Mazembe ni Shughuli

Mbwana Samatta

Mshambuliaji wa timu ya taifa ‘Taifa Stars Mbwana Samatta anayekipiga na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, amesema ushindani wa namba katika kikosi cha timu hiyo ni mkubwa sana, na nafasi anayocheza inawaniwa na washambuliaji watano toka mataifa yanayotambulika kisoka Duniani.

Spurs yakataa £40m za Chelsea kumsajili Modric

Luca Modric

Tottenham wamekataa ofa iliyotolewa na timu ya Chelsea ya £40 million, kwa ajili ya kumsajili kiungo wao Luka Modric, hii ni kwa mujibu wa meneja wa timu hiyo Harry Redknapp.

Ngog ajiunga na Bolton


David Ngog

Klabu ya Liverpool imethibitisha kwamba mchezaji wao David Ngog amejiunga na timu ya Bolton kwa mkataba wa miaka mitatu.

Ngog, 22, alijiunga na Liverpool kutoka Paris St Germain mnamo July 2008, amefanikiwa kucheza mechi 94 na kufunga magoli 19, ila alishindwa kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo, na hasa baada ya kuwasili kwa Luis Suarez na Andy Carroll mwezi January mwaka huu.

Taarifa kwenye mtandao wa Liverpool imesema: ''Kila mmoja hapa Liverpool FC anamtakia David kheri kwenye taaluma na maisha yake ya mbele.''

Manchester City yamsajili Owen Hargreaves



Manchester City imekamilisha usajili wa aliyekuwa mchezaji wa Manchester United Owen Hargreaves kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Diego Forlan ajiunga na Inter Milan


Diego Forlan

Klabu ya Inter Milan imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Atletico Madrid Diego Forlan

Forlan, 32, amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo, ikiaminika ujio wake ni kwa ajili ya kuziba pengo liliachwa na Samuel Eto'o.

''Diego, anakaribishwa Inter,'' inasoma taarifa kwenye mtandao wa klabu ya Inter.

Arsenal yamsajili Andre Santos


Andre Santos

Klabu ya Arsenal imethibitisha kuwa imemsajili beki wa ki-brazil Andre Santos toka klabu ya Fenerbahce kwa gharama ya Dolla Millioni 6.

Santos, mwenye miaka 28, anategemea kuongeza uzoefu kwenye kikosi cha Arsenal kilicho na wachezaji wengi makinda, inaaminika amesajiliwa ili kuweza kuziba pengo lililoachwa wazi na Gael Clichy, ambae alijiunga na timu ya Manchester City mnamo mwezi July.

Beki huyo ambaye pia amewahi kuichezeea timu ya Corinthians, amesema amefurahi kujiunga kwenye Ligi Kuu ya Uingereza akiwa amefata nyayo za wa Brazil wenzake kama Eduardo, Sylvinho, Denilson na Gilberto Silva ambao wamewahi kichezea Arsenal.

Scott Parker ajiunga Tottenham

Scott Parker

Klabu yaTottenham imefikia makubaliano ya kumsaini kiungo wa Uingereza Scott Parker toka West Ham.

Uhamisho huo, umekuja baada ya mchezaji huyo kuuandikia barua Uongozi wa West Ham juu ya nia yake ya kuhama klabu hiyo. Parker aliandinika, ningetamani nicheze kwenye Ligi kuu.

Ikumbukwe West Ham kwa sasa haipo kwenye Ligi Kuu ya Uingereza na hii ni baada ya kushuka daraja msimu uliopita.

Kiungo wa Liverpool Joe Cole Ajiunga na Lille kwa Mkopo


Joe Cole

Kiungo wa Liverpool Joe Cole, amejiunga na timu Lille ya Ufaransa kwa Mkopo ambao utamuweka huko kipindi chote cha msimu.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 jana Jumanne alisafiri kwenda Ufaransa kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya, inaelezwa kuwa Aston Villa nao walikuwa wanamtolea macho mchezaji huyo

Chelsea yakaribia kumnasa Pereira

Alvaro Pereira

Wakala wa mchezaji Alvaro Pereira anayekipiga na timu ya Porto, amesema wako kwenye mazungumzo na timu ya Chelsea juu uwezekano wa kumsajili mchezaji wake.

Bosi wa timu ya Blues Andre Villas-Boas anamfahamu vyema mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay toka kipindi walichokuwa pamoja cha Estadio do Dragao wakiwa na timu ya Porto, na sasa anataka kuungana tena na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 kabla ya dirisha la usajili halijafungwa.

Mchezaji huyo aliyewahi kuchezea CFR Cluj na Argentinos Juniors, kwa sasa anasubiri kusikia kiasi cha fedha kitakachopitishwa ili aweze kukamilisha usajili wake, na wakala wake Alejandro Savich kwa sasa yupo nchini Uingereza akishughulikia suala hilo.

Timu kama Barcelona, AC Milan na Inter Milan nazo zimetajwa kumtaka mchezaji huyo.

Hii ni mara ya pili kwa Chelsea kutaka kumsajili mchezaji huyo, baada ya maombi yao ya mara ya kwanza kutolewa nje.

Liverpool yakamilisha usajili wa Sebastian Coates

Sebastian Coates

Liverpool wamekamilisha usajili wa Beki wa Kimataifa wa Uruguay Sebastian Coates toka timu ya Nacional ya nchini humo.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20, ni mmoja kati ya wachezaji waliovutia kwenye kikosi cha Uruguay, ambapo aliiwezesha nchi yake kutwaa kombe la Copa mnamo mwezi July mwaka huu, haijaelezwa Coates amaesaini mkataba wa muda gani ila inaaminika amesaini mkataba wa muda mrefu na wana hao wa Anfiel.

Mchezaji huyo beki wa kati mwenye urefu wa nchi 6, amefaulu vipimo vya afya na pia ameweza kupata kibali cha kufanya kazi na timu ya Liverpool, kumfanya awe mchezaji wa 6 kusajiliwa na Liverpool katika kipindi hiki cha usajili cha majira ya joto chini ya Kenny Daglish.

Tuesday, August 30, 2011

Sneijder: Siondoki Inter Nabaki

Wesley Sneijder

Wesley Sneijder, hatimae amemaliza kile kilichokuwa kinaaminika kinaweza kutokea katika kipindi hiki cha uhumisho kinachomalizika kesho huko barani Ulaya, na hii baada ya leo hii kutangaza rasmi nia yake ya kuendelea kuichezea timu yake ya Inter Milan.

Sniejder kwa kipindi kirefu sasa amekuwa akihusishwa na kuhamia kwenye Ligi kuu ya Uingereza, huku timu za Chelsea, Manchester City na United zikiwa zinamfatilia kwa karibu.

Sneijder alieleza Sender Nos.  " Ninabaka hapa Inter, Sidhani kama nitaweza kuondoka katika kipindi hiki, Kuhusu Manchester United? Chochote kinaweza kutokea ila sidhani kama kuna lolote linaloweza kutokea kwa sasa.
"Najua kama ningepaswa kuondoka basi ingenibidi niondoke kwa bei muafaka, na hiyo ilikuwa wazi. Ila hakika sijawahi kuwa na mazungumzo rasmi na moja ya vilabu viwili vya Manchester.

Messi apewa Unahodha wa Argentina

Lionel Messi

Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Argentina Alejandro Sabella, amemkabidhi rasmi unahodha wa timu ya taifa ya Argentina nyota wa timu ya Barcelorna Lionel Messi.

Tofauti na anayokuwa na timu yake ya Barcelona, Messi amekuwa na wakati mgumu wa kuonyesha makali yake akiwa na timu yake ya taifa, akishindwa kuisaidia timu yake kwenye mashindano ya kombe la Dunia ya mwaka 2010 na yale ya Copa America yaliyoisha hivi karibuni nchini mwao.

Sabella, ambaye alichukua mikoba ya ukocha toka kwa Sergio Batista kama Kocha wa Argentina mwezi huu, ameanza kufanya mabadiko kwenye timu hiyo kwa kumvika kitambaa cha unahodha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, kitambaa ambacho hapo awali kilikuwa kinavaliwa na mchezaji wanayecheza nae timu moja ya Barcelona  Javier Mascherano, Argentina wanavaana na Venezuela siku ya Ijumaa.

Poulsen awaita 30 Kikosi cha Ngorongoro Heroes

Kikosi cha Ngorongoro Heroes

KOCHA wa timu za vijana, Kim Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 30 wa timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) kwa ajili ya mazoezi mwezi ujao.

Poulsen alitangaza majina hayo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Aliwataja wachezaji hao na timu zao katika mabano kuwa ni Saleh Ally (TSA), Jackson Wandwi (Azam), Hassan Kessy (Mtibwa Sugar), Khamis Mroki (Mtibwa Sugar), Yassin Mustapha (Polisi Dodoma), Andrew Kasembe (Moro United), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Ally Teru (Simba), Said Ruhava (Kagera Sugar) na Samuel Mkomola (Azam).

Wengine ni Frank Damayo (JKT Ruvu), Omega Seme (Yanga), Atupele Green (Yanga), Thomas Ulimwengu (ABC Sweden) na Jerome Lambele (Moro United).

Pia wapo Simon Msuvan (Azam), Ramadhan Singano (Simba), Alex Joseph (Majimaji), Ibrahim Rajab (Azam), Renatus Patrick (Polisi Dodoma), Abdallah Kilala (AFC), Rajab Zahir (Moro United), Amani Kyata (TSA), Edward Shija (Simba).

Wengine katika orodha hiyo ni Alfred Amede (Russia), Khelf Hassan (Kenya), Emily Mgeta (TSC Mwanza), Ramadhan Salum (Simba), Frank Sekule (Simba) na Hassan Dilunga (Ruvu Shooting).

Wachezaji Stars wanaocheza soka la kulipwa wawasili


Wachezaji  wa Stars wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi wamewasili kwenye kambi kwa ajili ya mchezo wa kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika dhidi ya Algeria utakaochezwa Jumamosi ijayo kwenye Uwanja wa Taifa.

Wachezaji waliowasili ni pamoja na Mbwana Samatta anayechezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, beki Idrissa Rajabu wa Sofapaka ya Kenya, Danny Mrwanda na Abdi Kassim wanaocheza soka la kulipwa nchini Vietnam katika klabu ya DT Long An, kiungo Henry Joseph wa Konsivinger ya Norway na Athumani Machupa wa Vasuland IF ya Sweden.

Wambura alisema kiungo wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa Canada katika klabu ya Vancouver Whitecaps, Nizar Khalfan anatarajiwa kuwasili leo usiku tayari kujiunga na kambi ya timu hiyo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Boniface Wambura alisema Kassim, Mrwanda na Samatta waliwasili juzi wakati Joseph, Rajabu na Machupa waliwasili jana. 

Liverpool wakataa ofa ya Chelsea kubadilishana na Raul Meireles

Timu ya Liverpool imetupilia mbali ofa ya Chelsea ya kumtaka mchezaji wao Raul Meireles, inaelezwa Chelsea walikuwa tayari kutoa Paundi Millioni 8 huku Yossi Benayoun akijumuishwa kwenye hesabu hiyo.

Meneja wa timu ya Chelsea Andre Villas-Boas alishawahi kufanya kazi na kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28 wakati walipokuwa pamoja na timu ya Porto, kabla ya mchezaji huyo kujiunga na Vijogo hao wa Anfield kwa ada ya Paundi Milioni 11 msimu uliopita.

Chelsea wameamua kutaka kumsajili Meireles baada ya kushindwa kwenye jaribio lao la kutaka kumsajili kiungo wa timu ya Tottenham Luka Modric.

Joe Cole njiani kujiunga na Lille kwa Mkopo

Mchezaji wa timu ya Liverpool Joe Cole yupo mbioni kujiunga na timu ya Lille ya nchini Ufaransa kwa mkopo wa msimu mzima.
Inaaminika Queens Park Rangers na Tottenham Hotspur nao wanamtolea macho mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29.

Arsenal kukamilisha usajili wa Per Mertesacker

Kocha wa timu ya Taifa ya Ujerumani Joachim Low amethibitisha kumpa ruhusa mchezaji wa timu hiyo Per Mertesacker kuondoka kwenye kambi ya timu hiyo ili aweze kwenda Lonon kukamilisha mpango wake Arsenal.

Mchezaji huyo beki wa timu ya Werder Bremen mwenye umri wa miaka 26 aitwae Mertesacker, anategemea kufanya vipimo na washika bunduki hao leo hii Jumanne, vipimo ambavyo kama akifaulu vitamuwezesha kujiunga moja kwa moja na timu hiyo inayoshiriki kwenye ligi kuu ya Uingereza.

Arsenal wakamilisha usajili wa Park Chu-Young

Klabu ya Arsena imethibitisha kwamba wamekubaliana na timu ya Monaco juu ya uhamisho wa mchezaji wa timu hiyo Chu Young Park.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 raia wa Korea ambaye pia ni Captain wa nchi hiyo, ameifungia timu ya Monaco jumla magoli 25 kwenye mechi 91 alizoichezea kwa misimu mitatu kwenye ligi ya nchi hiyo maarufu kama Ligue 1.
 
Mchezaji huyo amewahi kushinda tuzo ya mwanasoka chipukizi wa mwaka wa bara la Asia, alianza kuichezea timu ya taifa ya Korea akiwa na umri wa miaka 19, aliichezea timu yake ya taifa kwenye mashindano ya kombe la dunia ya mwaka 2006 na 2010. Kwa sasa mchezaji huyo ndiye Captain wa nchi yake na hii ni baada ya kuchukua nafasi ya captain aliyestaafu Ji Sung Park mapema mwaka huu.

Owen Hargreaves anajiandaa kujiunga na Man City?

Kuna uwezekano mkubwa kwa mchezaji aliyeachwa na Manchester United Owen Hargreaves kufanya uhamisho ambao watu wengi utaweza kuwashangaza, na hii ni baada ya ripoti uliyotoka leo hii ikieleza kuwa mchezaji huyo amefanya vipimo vilivyochukua masaa matatu kwenye hospitali ya timu ya Manchester City.

Picha iliyopigwa leo Jumanne na Gazeti la Sun la nchini Uingereza, imemuonyesha ya mchezaji huyo akitoka kwenye hospotali ya Bridgewater.

Monday, August 29, 2011

TFF yazidi kuiwekea ngumu Yanga

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema linapinga makubaliano yoyote baina ya Yanga na wadhamini wa Ligi Kuu, Kampuni ya simu ya Vodacom yenye lengo la kubadilisha rangi ya nembo kwenye jezi za timu hiyo na kusema watazingatia kanuni zinazoendesha ligi hiyo kuamua suala hilo.

Kauli hiyo ya TFF inafuatia kuwapo kwa taarifa kwamba, Uongozi wa Kampuni ya Vodacom na ule wa Yanga kwa pamoja umekubaliana kubadilisha rangi ya nembo iliyopo kwenye jezi za timu hiyo kutoka nyekundu na kuwa nyeusi ili kumaliza mgogoro ulioibuka baina ya pande hizo mbili kwa upande mmoja na shirikisho hilo kwa upande mwingine.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema hatua ya shirikisho hilo kuikubalia Yanga kubadilisha rangi ya nembo kwenye jezi za timu yao ni sawa na ukiukwaji wa kanuni za Ligi Kuu ambazo zinataka timu zote zinazoshiriki Ligi Kuu kuzifuata.

"Hatuwezi kukubali kuyumbishwa na timu moja, ikiwa tutaacha hali hii iendelee ni dhairi tunaweza kuwakimbiza wadhamini ambao wana nia njema ya kuendeleza soka hapa nchini.

"Sisi kama TFF tutakachoangalia hapa ni kanuni zinasemaje, kwa sababu ikiwa tutalichukulia hili suala juu juu na kuiruhusu Yanga kufanya inavyotaka inaweza kutuletea matatizo zaidi kwa sababu klabu nyingine zinaweza kujitokeza na kusema hazitaki hiki.

"Sio kweli kwamba viongozi wa klabu hizi hawajui mambo haya,wanafahamu vizuri masharti ya mdhamini isipokuwa wanafanya hivi kwa lengo la kutuyumbisha,"alisema Wambura bila kufafanua ni kanuni ipi watakayoitumia.

Hata hivyo Wambura alisema kuwa pande hizo tatu, yaani TFF,Vodacom na Yanga zitakuwa na kikao cha pamoja leo kwenye ofisi za shirikisho hilo ili kuzungumzia suala hilo.

Injured Drogba misses out

Didier Drogba will miss the Ivory Coast's match against Rwanda on Saturday as a result of the concussion he suffered against Norwich at the weekend.

Drogba had to be carried off on a stretcher after being accidentally hit on the head by Canaries goalkeeper John Ruddy while going for a header in the second half of the Blues' 3-1 win at Stamford Bridge on Saturday.
Drogba was due to travel to Africa on Monday to link up with his international team-mates, but he has stayed in London and will be monitored over the next few days by Chelsea's medical staff.

Barca begin with a bang

Barcelona began their bid for a fourth successive Primera Division title with a spellbinding 5-0 win against Villarreal at the Nou Camp.
Having been forced to wait to start their title defence, and after Real Madrid's 6-0 win at Real Zaragoza on Sunday, Pep Guardiola's side picked up where they left off last season to leave Juan Carlos Garrido's visitors dazed and confused.
Emerging midfielder Thiago started the scoring in the 25th minute before Cesc Fabregas, signed from Arsenal this summer, made it 2-0 on his league debut. Fellow newcomer Alexis Sanchez also marked his debut with a goal before Lionel Messi grabbed two for himself.
Fabregas lined up in midfield, with Chilean Sanchez wide on the right. Villarreal, fourth-place finishers last season, fielded first-choice duo Giuseppe Rossi and Nilmar up front.
Barcelona's first chance fell to Sanchez in the sixth minute but his shot was held well by Diego Lopez.
In the 17th minute the hosts forged another opportunity when Pedro slipped in Messi on the left and Lopez had to be alert to make the near-post save, before Sergio Busquets' header from the resulting corner bounced off the top of the bar.
The Catalan side's season was up and running when Thiago claimed the first goal of the season. The midfielder was allowed to carry the ball forward unopposed before simply firing the ball past Lopez with his left foot.
Rossi immediately burst into life and was not far off with a powerful shot at the other end.
The 38th minute saw Rossi go close, smashing a shot which Valdes saved only for the ball to bounce up on the line before the goalkeeper swiped it away. However, a raised flag confirmed Rossi had been ruled offside anyway.
The second goal came on the stroke of half-time and it was former youth team colleagues Messi and Fabregas at the heart of it. Argentinian Messi dropped deep to play an inch-perfect ball through to meet Fabregas' run and the homecoming Catalan nudged it around Lopez before tapping in.
Early in the second half Sanchez joined Fabregas as a goalscorer on his debut and this time Thiago was the provider, playing a delightful ball through the defence for Sanchez to race on to and place past Lopez with the measured finish.
Fabregas had another chance of his own seconds later as Barcelona continued to pile forward.
It was 4-0 in the 51st minute with a similarly incisive passing move, Iniesta playing a give-and-go before slotting through for Messi to round Lopez and score.
Fabregas was given an ovation when he was replaced by Jonathan Dos Santos in the 70th minute before Messi got his second of the night when he crashed home after a lovely one-two with Thiago.
Home goalkeeper Victor Valdes was alert when suddenly called on to deny Javier Camunas five minutes from time as Villarreal sought in vain for a positive to take from the match.

Tottenham wanataka kumsajili Owen

Inaelezwa kwamba Tottenham wako mbioni kumsajili kiungo aliyetupiwa virago na timu ya Manchester United Owen Hargreaves.

Arsenal, Liverpool na Lille wamsaka Yossi Benayoun

Arsenal, Liverpool na timu ya Ufaransa Lille, wameonyesha nia ya kutaka kumsajili kiungo wa Chelsea Yossi Benayoun.

Mchezaji  huyo raia wa Israel mwenye umri wa miaka 31hivi karibuni kupitia mtandao Twitter alieleza nia yake ya kuondoka kwenye timu hiyo ya Stamford Bridge.

Arsenal wanaonekana wako nia ya dhati kumchukua mchezaji huyo, ili wawaeze kuziba mapengo yaliyoachwa na wachezaji wake Cesc Fabregas na Samir Nasri.

Benayoun alijiunga na Chelsea toka Liverpool kwa thamani ya £5m, mnamo mwezi July 2010 huku akibahatika kupata nafasi ya ya kucheza kwa dakika moja tu toka msimu mpya uanze.

Algeria kuwasili leo kuikabili Star

Msafara wa watu 50 wa timu ya soka ya taifa ya Algeria unawasili nchini leo tayari kwa
ajili ya mchezo wa kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Septemba 3.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema kwamba Algeria itafika leo kwa ndege ya kukodi na baada ya kuwasili itaenda moja kwa moja katika hoteli ya Golden Tulip ambako watafikia.

Aidha, Wambura alisema kwamba waamuzi wote katika mchezo huo watatoka Mauritania huku kamisaa wa mchezo huo atakuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicolas Musonye.

Yanga watafuta mbadala wa Vodacom

Baadaa ya kugoma kuvaa jezi zenye nembo ya rangi nyekundu ya Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom kwenye mashindano ya Ligi Kuu ya soka Tanzania bara, Klabu ya Yanga imeanza mazungumzo na kampuni mbili za simu kwa ajili ya udhamini.

Yanga imekataa kuvaa jezi hizo huku sababu ikiwa nembo ya wadhamini wa ligi hiyo Vodacom kuwa ina rangi nyekundu ambayo ni ya mahasimu wao wa soka la Tanzania, Simba.

Gurumo jukwaa Idd Mosi

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini Muhidin Gurumo anatarajiwa kupanda jukwaani Idd Mosi mwaka huu akiwa na bendi yake ya Msondo Ngoma Music.

Gurumo hajaonekana jukwaani kwa muda mrefu sasa kutokana na kuwa mgonjwa, lakini Msondo imepanga bonanza maalumu litakalofanyika viwanja wa Sigara, Chang’ombe Dar es Salaam siku ya Idd el Fitri.

Arsenal kuwapa washabiki wake ofa ya tiketi za Bure

Club ya Arsenal imetangaza kuwapa ofa ya tiketi za bure washabiki wake waliohudhuria kwenye mechi ambayo iliisha kwa timu hiyo kufungwa na Man United kwa jumla ya magoli 8-2.

Imeelezwa inapata washabiki 3,000 walisafiri umbali wa Maili 400 kwenda kuona mchezo huo, ambao uliisha kwa kipigo cha aibu kwa timu yao.

Taarifa toka Club hiyo zimesema, mashabiki wa timu hiyo waliohudhulia mechi hiyo watapewa ofa hiyo kwenye moja kati ya mechi za ugenini itakayochezwa na timu hiyo.

Wenger apologises for United mauling

Arsene Wenger has apologised to the Arsenal fans for their humiliating defeat at Old Trafford on Sunday.
The Gunners conceded eight goals for the first time since 1896 as they suffered a catastrophic 8-2 loss at Manchester United.
It was a result that prompted extreme criticism from fans and pundits alike, but Wenger has insisted he will not walk away from what is clearly a massive job to rebuild the confidence of a club who are still to find replacements for Cesc Fabregas and Samir Nasri, and have collected just a single point from their three Premier League games so far.
The Arsenal boss has pledged to try and find some new players ahead of the transfer window closing on Wednesday night. However, for now, the best he can do is say sorry.
''The fans do not want to see their team like that,'' Wenger told Arsenal World. ''We can only apologise and come back in our strength and desire in the next game.
''Big scores are humiliating and difficult to swallow but I don't think they have a special meaning. They are always under special circumstances.''
For Wenger, those special circumstances were a lengthy injury list, which robbed him of the services of Jack Wilshere, Thomas Vermaelen and Bacary Sagna amongst others, plus the suspensions of Alex Song, Gervinho and Alex Frimpong.
The visit of Swansea immediately after the international break offers the perfect opportunity for a morale-boosting victory, although for now, skipper Robin van Persie accepts his team-mates have to face up to some pretty harsh facts.
''It is an honest result if you look at the game,'' said the Gunners captain. ''It sounds crazy maybe but Manchester United were much better than us and they punished us hard.
''We were simply not good enough. We have to deal with that. I don't think we can hide behind injuries or suspensions. It is no excuse. They had injuries too, this is football.''

ARRIVEDERCI DIEGO FORLAN - THANKYOU

The 32 year old Uruguayan International DIEGO FORLAN has said officially goodbye to SPANISH FOOTBALL & to all the ATLETICO DE MADRID fans in a Press Conference this afternoon. The player is on the verge of shutting the final details with Italian Club INTER MILAN. As an Atletico de Madrid fan & follower I can only give publicly my sincere thanks to Forlan for the services given to the Club during his stay:
  • 96 goals in 198 official games
  • European Golden boot 2009 - 2010 with 32 goals
  • Europa League Champion 2010 
  • European Super Cup 2010


Friday, August 26, 2011

Man City wakamilisha usajili wa Nasri

Club ya manchester City imekamilisha rasmi usajili wa aliyekuwa kiungo wa Arsenal Samir Nasri, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 amesaini mkataba wa miaka 4 pale Etihad, vyanzo vya karibu vimesema dau lililotumika kumnasa kiungo huyo linakadiliwa kuwa kiasi cha paundi Millioni 24.

Pia imeelezwa kwamba mchezaji huyo wa kifaransa anategemea kuwemo kwenye mechi ya jumapili ambapo Man city watacheza na timu ya Tottenham kwenye uwanja wa White Hart Lane, na atakuwa anavaa jezi namba 19.

Tottenham wakabidhiwa wabaya wao

Klabu ya soka ya Tottenham ya Uingereza ambayo msimu uliopita ilishiriki Ligi ya mabingwa wa Ulaya na kuchachafya baadhi ya vigogo kabla ya kutolewa na Real Madrid, itajaribu tena bahati yake katika michuano ya Ulaya msimu huu kwa kuumana na Rubin Kazan, PAOK Salonika, pamoja na Shamrock Rovers.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa jioni ya leo na shirikisho la vyama vya soka barani Ulaya (UEFA), kwa michuano ya ligi ya washindi barani humo, Spurs wako kundi A, sanjari na timu hizo, na wadadisi wa masuala ya soka wameonyesha wasiwasi wao kwa kulielezea kundi hilo kuwa si rahisi kama ambavyo linaweza kuonekana machoni mwa watu kwa kusoma.
Katika ratiba hiyo, timu nyingine za Uingereza za Stoke City, Fulham, pamoja na Birmingham, nazo zimepangwa katika makundi tofauti tofauti, huku pia makundi yao yakielezwa kuwa si mchekea.
Makundi hayo kwa mujibu wa UEFA ni kama ifuatavyo:
Group A: TOTTENHAM, Rubin Kazan, PAOK Salonika, SHAMROCK ROVERS
Group B: FC Copenhagen, Standard Liege, Hannover, Vorskla Poltava
Group C: PSV Eindhoven, Hapoel Tel-Aviv, Rapid Bucharest, Legia Warsaw
Group D: Sporting Lisbon, Lazio, FC Zurich, FC Vaslui
Group E: Dynamo Kiev, Besiktas, STOKE, Maccabi Tel-Aviv
Group F: Paris St Germain, Athletic Bilbao, Salzburg, Slovan Bratislava
Group G: AZ Alkmaar, Metalist Kharkiv, Austria Vienna, Malmo
Group H: Braga, Club Brugge, BIRMINGHAM, Maribor
Group I: Atletico Madrid, Udinese, Rennes, Sion
Group J: Schalke, Steaua Bucharest, Maccabi Haifa, AEK Larnaca
Group K: FC Twente, FULHAM, Odense, Wisla Krakow
Group L: Anderlecht, AEK Athens, Lokomotiv Moscow, Sturm Graz

Baada ya kipigo cha Simba…Wachezaji na mashabiki Yanga wafanya fujo

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida wachezaji wa Yanga, Jerryson Tegete, nahodha Shadrack Nsajigwa na Nadir Haroub baada ya kumalizika kwa mechi ya kuwania Ngao ya Jamii dhidi ya Simba iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam walivamia gari la Waandishi wa habari wa Mwananchi lililokuwa katika foleni ya kutoka uwanjani humo na kuanza kufanya fujo.
Tegete alifanya vurugu hizo baada ya kuambiwa na mtu asiyekuwa mwandishi wa gazeti la Mwananchi kwamba wamefungwa 2-0, lakini kwa sababu mtu huyo alikuwa ndani ya gari la Mwananchi, mshambuliaji huyoalishuka kutoka kwenye basi la Yanga na kupiga kwa nguvu kioo cha nyuma cha basi la Mwananchi kabla ya kufungua mlango wa gari na kuingia ndani ya gari la Mwananchi.
Mshambuliaji huyo alikuwa akifuatana na nahodha wake Shadrack Nsajigwa aliyekuwa akimzuia, lakini Tegete alianza kufanya fujo kwa kumshambulia mtu huyo aliyekuwa ndani ya basi hilo pamoja na waandishi wa Mwananchi na waandishi wengine wa habari.
Mpiga picha wa gazeti hili, alipojaribu kumpiga picha Tegete wakati akifanya fujo Nsajigwa akataka kumnyang’anya kamera mpiga picha ili asipige tukio hilo, hali iliyosababisha kuhamasisha vurugu kwa mashabiki waliokuwapo kutaka kupora kamera, kompyuta na simu za waandishi zilizokuwapo kwenye gari.
Wakati Tegete na Nsajigwa wakifanya fujo hizo Haroub ‘Canavaro’, alitumia mwanya wa dereva wa Mwananchi aliyekuwa ameshuka kukagua gari kama limevunjwa kioo na yeye kukaa kwenye kiti cha dereva huku akijaribu  kuwasha gari hilo, lakini jitihada zake Nadir ziligonga mwamba baada ya mwandishi Jackson Odoyo wa Mwananchi aliyekuwa kwenye kiti cha mbele kung’ang’ania funguo na kumkamata mikono mpaka dereva aliporejea na kuuchukua ufunguo huo.
Hata hivyo; katika fujo hizo mwandishi wa habari wa gazeti la Jambo Leo aliyekuwa ndani ya gari la Mwananchi, Julius Kihampa alipoteza simu yake ya kiganjani aina ya Nokia.
Katika hatua nyingine mashabiki wa Yanga Bombaa juzi usiku walimvunja mkono mwanachama wa Simba,  Salum Cheusi aliyekuwa akisheherekea ushindi wa timu yake.
Cheusi alijikuta matatizoni baada ya songombingo kuibuka uwanjani kati ya wanachama wa Yanga na Simba waliokuwa wakilinda uwanja wa Taifa wakihofia kufanyiwa vitendo vya ushirikina.
Mbali na Cheusi mwanachama mwingine wa Simba anayefahamika kwa jina la Macho pia alijikuta akipewa kipigo kilichosababisha achanike mdomo kwa madai kuwa amekuwa akiihujumu Simba kwa kutoa taarifa za kila kinachoendelea ndani ya klabu hiyo.
Akizungumza na Mwananchi Macho alisema, “Kuna wataalum waliletwa na mzee …(jina limeifadhiwa) kutoka Zanzibar na walinzi walipewa shilingi 300,000 ili wawaruhusu kuingia uwanjani na fedha hizo mimi ndio nilipewa niwape,”alisema mwanachama huyo.
“Tulikuwa kundi la watu 30 sikupigwa na wanachama wa Simba nilipigwa na Yanga bomba wakiongozwa na Shamte Mkumba, nilipigwa nikiwa naongea na simu nikipokea maelekezo kutoka kwa mzee kuhusu wataalamu wetu.
“Ilikuwa ni saa saba usiku walimpiga Cheusi na kumvunja mkono hata kesho utamuona amevaa P.O.P,  lakini masuala yote haya viongozi wameshayamaliza.”

Vodacom Miss Tanzania wazuru kaburi la Sokoine

WAREMBO 30 wanaowania taji la Vodacom Miss Tanzania, wametakiwa kuwa mabalozi na kioo kwa jamii inaowazunguka ili kuipa sifa fani hiyo, ambayo watu wengi wanaona imejaa uhuni wakati si kweli.
Ushauri huo umetolewa na diwani wa Kata ya Monduli Juu iliyopo wilayani Monduli mkoani Arusha, Bariki Sumuni wakati warembo hao walipozuru kaburi la Waziri Mkuu wa zamani hayati Edward Sokoine.
Sumuni alisema watu wengi na hasa jamii ya kimasai ilikuwa na mtazamo tofauti na mashindano ya urembo, kwani baadhi ya warembo wanapotwaa taji la MissTanzania wanafanya vitu ambavyo ni kinyume na maadili na kufanya wazazi kuendelea kuchukia fani.
Alisema kwa sasa jamii ya kifugaji ya Kimasai imeanza kuelimika ikiwa ni pamoja na kuwaruhusu watoto wao wa kike kwenda shule na hata kushiriki urembo tofauti na zamani, hivyo basi huenda miaka ijayo Miss Tanzania anaweza kuwa jamii ya kimasai na kuwakilisha
vema nchi.
‘’Sisi Wamasai watoto wa wetu wa kike zamani tulikuwa hatutaki hata waende shule, lakini kwa sasa wazazi tuko mstari wa mbele kuhakikisha watoto wetu wanaenda shule na hata kushiriki urembo,’’ alisema.
Diwani huyo aliwasifu warembo hao kwa uamuzi wao wa kulitembelea kaburi la Sokoine, kwani ni uamuzi mzuri na wanapaswa kuuenzi kwa kuiga mifano ya marehemu huyo ikiwa ni pamoja na kuiga yaliyokuwa yakifanywa enzi za uhai wake.
Alisema hayati Sokoine alikuwa muadilifu, mcha Mungu na alikuwa mstari wa mbele kulinda maadili ya mtoto wa kike kwa kujiheshimu, hivyo basi warembo hao wanapaswa kuiga mfano huo, ikiwa ni njia mojawapo ya kumuenzi kutembelea kaburi hilo.
Warembo hao pia walitembelea kampuni ya Tan Media inayomiliki kituo cha redio 5 na TV ya ABC kuijionea wenyewe namna ya uandaaji na utangazaji unaofanywa na watangazaji wa kampuni hiyo.

Mtukutu Joey Barton atua rasmi QPR

Kiungo mtukutu, ambaye katika siku za karibuni amekuwa kwenye mgogoro wa kinidhamu na uongozi wa klabu ya Newcastle, Joey Barton ameachana rasmi na klabu hiyo na kutua Queens Park Rangers.
Barton mwenye miaka 28, ambaye alitua Newcastle akitokea Manchester City mwaka 2007, alikuwa katika mwaka wa mwisho wa mkataba wake na mapema baada ya kufunguliwa kwa dirisha la usajili msimu huu, aliwekwa sokoni baada ya kutumia mtandao wa kijamii wa Twitter kuwazodoa viongozi wake.
Wakati mchezaji mwenyewe akizungumzia uhamisho huo kama jambo muhimu lililohitajika ili kuhakikisha kuwa sakata lake na Newcastle linafikia ukingoni, taarifa fupi ya klabu ya QPR aliyojiunga nayo imeelezea usajili huo kuwa ni kwa ajili ya “kumuwezesha Barton, kuuonyesha ulimwengu wa soka kuwa yeye ni mchezaji mkubwa na atawaonyesha kile anachoweza kukifanya kwa ufasaha akiwa klabuni hapa”
Dau kamili la kiungo huyo mahiri lakini ambaye utukutu wake umekuwa ukimfanya aonekane mchezaji asiye na maana ndani na nje ya uwanja, halikutajwa lakini ni wazi kuwa QPR kama wataamua kuachana na matatizo yake ya nje ya uwanja na kutaka kunufaika na kile anachoweza kukifanya awapo uwanjani, watakuwa wamepata mmoja wa wachezaji muhimu watakaowapa nafasi ya kufanya vyema msimu huu.


Adebayor atua Spurs kwa mkopo

Klabu ya soka ya Tottenham, imethibitisha kuwa imefanikiwa kumsajili mchezaji wa zamani wa mahasimu wao wakuu, Arsenal, Emanuel Adebayor, kwa mkopo toka klabu ya Manchester City.
Usajili wa Adebayor, umekuja katika kipindi ambacho alikuwa kwenye hatihati ya kutokuwa na timu maalum ya kuchezea baada ya kocha wa Manchester City, Roberto Mancini, kunukuliwa hivi karibuni akisema kuwa mshambuliaji huyo raia wa Togo, hakuwa tena na nafasi katika kikosi chake.
Adebayor mwenye umri wa miaka 27, alitua Manchester City kwa dau nono la paundi za kiingereza milioni 25 mwaka juzi lakini ghafla akakosa namba katika kikosi hicho na alitumia msimu uliopita akiitumikia Real Madrid ya Uhispania kwa mkopo, ambapo wakati wa kampeni ya miamba hao wa Hispania katika Ligi ya mabingwa wa Ulaya, Adebayor akiwa na kikosi cha Madrid, aliwatungua Spurs kwa mabao mawili na kuchangia kuwaondoa katika mashindano hayo.


Afrika Kusini mwenyeji wa KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA 2013 badala ya LIBYA


Afrika ya Kusini imesema wao ndio watakao kuwa wenyeji wa Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2013 badala ya Libya.

Nchi hizo mbili zimefikia makubaliano hayo huku zikibadilishana haki ya kuandaa mashindano hayo, hiyo ikimaanisha kwamba Libya itaandaa mashindano ya mwaka 2017 ambayo yalikuwa yandaliwe na Afrika ya... Kusini.

Dili hilo lilitangazwa na Chama Cha Soka cha Afrika ya Kusini (Safa), na suala hili sasa linasubiri ridhaa ya Chama Cha Soka Afrika (Caf).

Maandalizi ya Libya kuandaa michuano hiyo kwa mwaka 2013 yamekuwa kwenye mashaka kwa kipindi sasa, na hii ni kutokana na vurugu zinazoendelea nchini humo kwa sasa.
See More

VICTOR COSTA AREJESHWA STARS


Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen leo (Agosti 25 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili ya mechi ya mchujo dhidi ya Algeria ‘Desert Warriors’ kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon.
Wachezaji walioitwa ni makipa Shabani Dihile (JKT Ruvu Stars), Juma Kaseja (Simba) na... Shabani Kado (Yanga). Mabeki wa pembeni ni nahodha Shadrack Nsajigwa (Yanga), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya) na Amir Maftah (Simba). Mabeki wa kati ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba) na Victor Costa (Simba).

Viungo wakabaji ni Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Juma Seif (Yanga) na Jabir Aziz (Azam). Viungo washambuliaji ni Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam) na Salum Machaku (Simba).

Washambuliaji ni Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Ramadhan Chombo (Azam), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden) na John Bocco (Azam).

Timu itaingia kambini Jumapili (Agosti 28 mwaka huu) mchana na jioni itaanza mazoezi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. Mechi dhidi ya Algeria itachezwa Septemba 3 mwaka huu kuanzia saa 10.00 jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam

Droo la makundi UEFA Champions League, Man City yapangwa kundi gumu

MAKUNDI KWA UJUMLA

Group A:
Bayern Munich, Villarreal, Manchester City, Napoli

Group B:
Inter Milan, CSKA Moscow, Lille, Trabzonspor

Group C:
Manchester United, Benfica, Basel, Otelul Galati

Group D:
Real Madrid, Lyon, Ajax, Dinamo Zagreb

Group E:
Chelsea, Valencia, Bayer Leverkusen, Genk

Group F:
Arsenal, Marseille, Olympiakos, Borussia Dortmund

Group G:
Porto, Shakhtar Donetsk, Zenit St Petersburg, APOEL Nicosia

Group H:
Barcelona, AC Milan, BATE Borisov, Viktoria Plzen

HAPA KUNA MCHEZAJI YUPI HAKUWAHI KUANDALIWA NA MAXIMO?

HAPA KUNA MCHEZAJI YUPI HAKUWAHI KUANDALIWA NA MAXIMO?

Shabani Dihile (JKT Ruvu Stars), Juma Kaseja (Simba) na Shabani Kado (Yanga). Mabeki wa pembeni ni nahodha Shadrack Nsajigwa (Yanga), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya) na Amir Maftah (Simba). Mabeki wa kati ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba) na Victor Costa (Simba).

Viungo wakabaji ni Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Juma Seif (Yanga) na Jabir Aziz (Azam). Viungo washambuliaji ni Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam) na Salum Machaku (Simba).

Washambuliaji ni Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Ramadhan Chombo (Azam), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden) na John Bocco (Azam).