Wednesday, August 31, 2011

Bellamy Arejea Liverpool

Craig Bellamy

Klabu ya Liverpool imethibitisha kumsajili mchezaji aliyewahi kuichezea timu hiyo Craig Bellamy.



Mchezaji huyo ambaye ni nahodha wa Wales, amerudi tena Anfield kwa mkataba wa miaka miwili baada kuwa huru toka Manchester City.

Bellamy ambaye aliondoka Liverpool baada ya msimu wa 2007 na kujiunga na West Ham, inaaminika atasaidia kuongeza nguvu ya ushambuliaji kwenye kikosi cha Kenny Dalglish, akiwa mchezaji wa ziada nyuma ya Luis Suarezna Andy Carroll.

No comments:

Post a Comment