Wednesday, August 31, 2011

Ngog ajiunga na Bolton


David Ngog

Klabu ya Liverpool imethibitisha kwamba mchezaji wao David Ngog amejiunga na timu ya Bolton kwa mkataba wa miaka mitatu.

Ngog, 22, alijiunga na Liverpool kutoka Paris St Germain mnamo July 2008, amefanikiwa kucheza mechi 94 na kufunga magoli 19, ila alishindwa kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo, na hasa baada ya kuwasili kwa Luis Suarez na Andy Carroll mwezi January mwaka huu.

Taarifa kwenye mtandao wa Liverpool imesema: ''Kila mmoja hapa Liverpool FC anamtakia David kheri kwenye taaluma na maisha yake ya mbele.''

No comments:

Post a Comment