Wednesday, August 31, 2011

Liverpool yakamilisha usajili wa Sebastian Coates

Sebastian Coates

Liverpool wamekamilisha usajili wa Beki wa Kimataifa wa Uruguay Sebastian Coates toka timu ya Nacional ya nchini humo.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20, ni mmoja kati ya wachezaji waliovutia kwenye kikosi cha Uruguay, ambapo aliiwezesha nchi yake kutwaa kombe la Copa mnamo mwezi July mwaka huu, haijaelezwa Coates amaesaini mkataba wa muda gani ila inaaminika amesaini mkataba wa muda mrefu na wana hao wa Anfiel.

Mchezaji huyo beki wa kati mwenye urefu wa nchi 6, amefaulu vipimo vya afya na pia ameweza kupata kibali cha kufanya kazi na timu ya Liverpool, kumfanya awe mchezaji wa 6 kusajiliwa na Liverpool katika kipindi hiki cha usajili cha majira ya joto chini ya Kenny Daglish.

No comments:

Post a Comment