Tuesday, August 30, 2011

Sneijder: Siondoki Inter Nabaki

Wesley Sneijder

Wesley Sneijder, hatimae amemaliza kile kilichokuwa kinaaminika kinaweza kutokea katika kipindi hiki cha uhumisho kinachomalizika kesho huko barani Ulaya, na hii baada ya leo hii kutangaza rasmi nia yake ya kuendelea kuichezea timu yake ya Inter Milan.

Sniejder kwa kipindi kirefu sasa amekuwa akihusishwa na kuhamia kwenye Ligi kuu ya Uingereza, huku timu za Chelsea, Manchester City na United zikiwa zinamfatilia kwa karibu.

Sneijder alieleza Sender Nos.  " Ninabaka hapa Inter, Sidhani kama nitaweza kuondoka katika kipindi hiki, Kuhusu Manchester United? Chochote kinaweza kutokea ila sidhani kama kuna lolote linaloweza kutokea kwa sasa.
"Najua kama ningepaswa kuondoka basi ingenibidi niondoke kwa bei muafaka, na hiyo ilikuwa wazi. Ila hakika sijawahi kuwa na mazungumzo rasmi na moja ya vilabu viwili vya Manchester.

No comments:

Post a Comment