Wednesday, August 31, 2011

Arsenal yamsajili Andre Santos


Andre Santos

Klabu ya Arsenal imethibitisha kuwa imemsajili beki wa ki-brazil Andre Santos toka klabu ya Fenerbahce kwa gharama ya Dolla Millioni 6.

Santos, mwenye miaka 28, anategemea kuongeza uzoefu kwenye kikosi cha Arsenal kilicho na wachezaji wengi makinda, inaaminika amesajiliwa ili kuweza kuziba pengo lililoachwa wazi na Gael Clichy, ambae alijiunga na timu ya Manchester City mnamo mwezi July.

Beki huyo ambaye pia amewahi kuichezeea timu ya Corinthians, amesema amefurahi kujiunga kwenye Ligi Kuu ya Uingereza akiwa amefata nyayo za wa Brazil wenzake kama Eduardo, Sylvinho, Denilson na Gilberto Silva ambao wamewahi kichezea Arsenal.

No comments:

Post a Comment