Tuesday, August 30, 2011

Messi apewa Unahodha wa Argentina

Lionel Messi

Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Argentina Alejandro Sabella, amemkabidhi rasmi unahodha wa timu ya taifa ya Argentina nyota wa timu ya Barcelorna Lionel Messi.

Tofauti na anayokuwa na timu yake ya Barcelona, Messi amekuwa na wakati mgumu wa kuonyesha makali yake akiwa na timu yake ya taifa, akishindwa kuisaidia timu yake kwenye mashindano ya kombe la Dunia ya mwaka 2010 na yale ya Copa America yaliyoisha hivi karibuni nchini mwao.

Sabella, ambaye alichukua mikoba ya ukocha toka kwa Sergio Batista kama Kocha wa Argentina mwezi huu, ameanza kufanya mabadiko kwenye timu hiyo kwa kumvika kitambaa cha unahodha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, kitambaa ambacho hapo awali kilikuwa kinavaliwa na mchezaji wanayecheza nae timu moja ya Barcelona  Javier Mascherano, Argentina wanavaana na Venezuela siku ya Ijumaa.

No comments:

Post a Comment