Tuesday, August 30, 2011

Liverpool wakataa ofa ya Chelsea kubadilishana na Raul Meireles

Timu ya Liverpool imetupilia mbali ofa ya Chelsea ya kumtaka mchezaji wao Raul Meireles, inaelezwa Chelsea walikuwa tayari kutoa Paundi Millioni 8 huku Yossi Benayoun akijumuishwa kwenye hesabu hiyo.

Meneja wa timu ya Chelsea Andre Villas-Boas alishawahi kufanya kazi na kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28 wakati walipokuwa pamoja na timu ya Porto, kabla ya mchezaji huyo kujiunga na Vijogo hao wa Anfield kwa ada ya Paundi Milioni 11 msimu uliopita.

Chelsea wameamua kutaka kumsajili Meireles baada ya kushindwa kwenye jaribio lao la kutaka kumsajili kiungo wa timu ya Tottenham Luka Modric.

No comments:

Post a Comment