Monday, September 5, 2011

Del Piero: Bado sijaamua mwisho wangu

Alessandro Del Piero

Mchezaji mkongwe wa Juventus Alessandro Del Piero, amesema bado hajaamua kama ataendelea kucheza mpira baada ya msimu huu wa 2011-12.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36, bado yupo kwenye mkataba unaomuweka mpaka mwezi June mwakani pale Turin, ila inaelezwa kwamba mwisho wa mkataba huo haimaanishi kwamba na yeye atastaafu.

"Kufikiria juu ya mwisho wangu kwenye soka , si kitu ambacho kinanichukulia muda kuamua. Bado sijaamua kama huu utakuwa ni mwisho wangu kucheza na Juventus," Del Piero alieleza La Gazzetta dello Sport.

"Kufikiria juu ya kwamba huu ni mwaka wangu wa mwisho inanifanya nijitoe kwa zaidi ya asilimia 200. Nahitaji kumaliza kipindi changu kwenye mafanikio ya juu.  Nikijaribu kuangalia nyuma miaka 20 iliyopita, nitaangalia nikiwa nimeridhika sana."

Del Piero alianza kucheza kwenye kiwango cha juu akiwa Padova, ila akajiunga na Juventus mnamo mwaka 1993. Mchezaji huyo mpaka sasa ameweza kucheza jumla ya mechi 600 kwa timu hiyo ya Serie A.

No comments:

Post a Comment