Sunday, September 4, 2011

Barcelona: Fabregas Ana Thamani ya £53m

Cesc Fabregas  

Makamu wa Rais wa Klabu ya Barcelona Josep Maria Bartomeu, anaamini kwamba Cesc Fabregas ana thamani ya £53ml, hela ambayo klabu yake ya awali Arsenal ilikuwa inahitaji kuweza kumuuza mchezaji huyo kwa Barca.

Makamu wa Rais huyo amesema, katika kipindi kifupi alichomuona akiitumikia Barcelona na Hispania kwa ujumla, amemkubali sana.

"Baada ya kuona kazi anayoifanya toka awasili hapa, hakika Cesc thamani yake inafika €60ml sawa na £53ml ambazo Arsenal walizihitaji," alisema Bartomeu. "Kijana anacheza kwa kiwango cha juu, na katika kipindi cha wiki tatu ya mazoezi uwezo wake ni wakushangaza . Hakika uhamisho huu ni mzuri, kimasoko hii iko wazi, si yakuficha Cesc ana thamani ya hela nyingi sana.

No comments:

Post a Comment